Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2022

SAA ZA MWISHO EPISODE 2

Picha
SAA ZA MWISHO ****Ep2*** S.P.Owino Mda ulizidi kusogea tititi! Mshale wa saa ya ukutani ulisogea, mama Kaka na dada Helena walipewa sehem wapumzike usikuule! Bila kufaham kilicho tokea kwa mgonjwa wao! Ilitimia saa 7:00 usiku Vipimo vikiwa vina onyesha kwamba tayari nilisha fariki, nilistuka moyo ukiwa kasi kweli nilihisi kizunguzungu na kichefuchefu mpaka nikatapika taa zilikua zime Zima hospitali nzima kimya. Nilijaribu kukohoa sauti ilikua kubwa Sana kwani nilikua mwenyewe nilie toa sauti. Niliogopa kidogo kwani kulikua na giza niliamka nikapapase ukuta ili nitafute switch niwashe taa, niligusa bila mafanikio ghafla taa iliwaka ndipo nilipo iona ile sura ya nesi Alie kua na mavazi ya kutisha nilitaka kupiga yowe ohooo! Kumbe siwezi kuongea tena ulimi wangu ulikua mzito. Alinisogelea aka niambia wewe niwakwetu na tumekupa siku tano ili ukubali kujitoa kwetu kwa ihari yako na hauta kiona kifo" una siku tano za kua hai ndani ya hospital hii Yani masaa 124, aliupanua mdomo wake a...

JUNE 17 EPISODE 2

Picha
JUNE 17 **Ep2** S.P.Owino Akiwa ndani ya kanisa aliendelea kusimulia kilicho tokea usiku ule anasema nilihisi watu wawili wakiongea sebleni niliamka na kapapasa ukuta niweze kuziwasha taa, lo! Kumbe umeme ulikua umekata ilinibidi niiwashe tochi ya sim yangu nikisoa taratibu sebuleni! Nilikua na usingizi Ila ilinibidi kwasababu ndio kaziyangu kuangalia nyumba wakiwa wamelala! Nilipo fika sebleni mh! Amelala mke wabosi Ila mtoto mdogo wa mwaka mmoja alikua macho halii alikua akinitazama tu usoni! Nilimuamsha mama mama amka aliamka akaniuliza saa ngapi nilimjibu saizi saa 8:23 usiku mtoto anang'atwa na mbu mpeleke kwenye neti nakumbuka aliniambia saw embu we kalale Kuna kipindi nilikua nakisubiri Ila kimesha nipita kumbe nilipitiwa na usingizi, aliniomba nikalale. Ilinibidi nirudi chumbani kwangu nilifunga mlango, nilipo tizama nje dirisha la chumba changu niliona taa a kiwaka! Sasa kwanini kwetu umeme hamna sikuchukulia maanani kwani yawezekan unit zimeisha japo hua Ningumu Sana Jamb...

MPENZI CLARA EPISODE 2

Picha
MPENZI CLARA EPISODE (02)✓ ILIPOISHIA..... Okay Sarah hapa tuliokutana jana usiku pale maeneo ya mwembe yanga wewe sindo (JOH) eeehe?!! ENDELEA NAYO SASA Oooh!!! kumbe ndio yule mrembo wa jana usiku uliechukua namba yangu pale njiani eeeh?! sema sorry nipe kama 2 minutes alafu nitakupigia maana saizi kuna mizigo naifatilia hapa (Airport) okay mrembo?! (SARAH- okay poa) alikata simu Baada kama ya dakika 25 nilitoka njee ya !Airport) na mizigo yangu yule dereva boda sasa daaaah (DEREVA BODA- bro mbona slow sana fanya chap chap basi tuondoke maana nimepigwa na jua sana hapa alafu inabidi tuongeze boda nyingine kwajili ya hiyo mizigo yako au mimi nitangulie na mizigo alafu wewe utapanda dala dala) ALIMALIZA KUONGEA Aaaah!!! bro na wewe mbona unakua unaongea sana kama ka-mtu kaaah (IRINGA) humo ndani kuna process unapitia mpaka kupata mzigo wako kwaiyo hauwezi kuingia tu nakutoka kama choo cha bar kwaiyo wewe funga hii mizigo kisha me nikaitisha boda nyingine na safari ikaanza ya kuelekea ...

DENI LA MAISHA SEHEMU YA 3

Picha
DENI LA MAISHA SEHEMU YA 03 GREAT MAN Hakua na sehemu ya kwenda kwani kipindi kile anasoma kwenye chuo cha elimu ya biashara alikua ni mtu wa kuja tu kutoka mkoani Miaka ishirini imepita hajui kwao kama ndugu zake ni wazima au wamekufa, john akiwa na sura ya makunyanzi iliyoanza kuzeeka, nywele zilizokaa muda mrefu bila kunyolewa na kufanyiwa usafi lakini nguo zake za muda mrefu zilizochoka zilifanya haonekane kama kichaa ndani ya jiji la dar es salaam. Kwa muda huo akili ya john ilikua kwa sara tu mwanamke ambae haujui familia yake wala hakujui kwao, aliamua kujitoa muanga na kubeba kesi nzito kwa ajili ya upendo wake na sasa aliona wakati umefika wa yeye kupata malipo yake kutokana na wema aliofanya. John hakutaka kurudi kwao na kwenda kuangalia maisha mengine, mawazo yake yalikua kwa sara, aliamini baada ya kuteseka miaka ishirini gerezani sasa ni muda wake wa kufurahia maisha akiwa na sara mwanamke anaempenda kuliko kitu chochote. Siku zilipita, john alikua analanda landa mitaani k...

NILIZAA NA KUOLEWA NA SHEMEJI KUMKOMOA MME WANGU PART: 02

Picha
NILIZAA NA KUOLEWA NA SHEMEJI KUMKOMOA MME WANGU PART: 02. Ilipoishia, Baada ya kumpigia, nilimueleza mwanzo mpaka mwisho ndipo aliponijibu, "Pole sana kwa hilo! mda huu nipo kazini lakini nimeamua kuacha kazi ili nikakusaidie" "Asante sana shemeji" nilimshukuru sana huku nikiomba afike mapema maana nilikuwa nimebanwa na haja kubwa. Baada ya mda kidogo, niliamua kuchungulia kama wameshaondoka lakini walikuwa bado wamenisubiria. Niliendelea kufunga  mlango huku nikisubiri msaada kutoka kwa shemeji yangu Julius. SONGA NAYO... Niliendelea kumsubiri shemeji mpaka mda ukawa unaenda sasa ndipo nilipomoigia simu kwa mara nyingine tena. Wakati nampigia simu, kumbe alikuwa karibu na mlango ndipo aliponiambia nifungue mlango. Nilijifunga kidedea kisha nikafungua mlango ndipo vurugu kali ilipoanza ambayo ilifanya kivumbi kikali kutimuka. "Mnafanya nini hapa! hamna kazi za kufanya! ngoja niwaoneshe kazi sasa" Shemu Julius akiwa na fimbo ya kunesanesa aliwambia wadogo ...

ZOMBI WA DAR EPISODE 2

Picha
ZOMBI WA DAR ABELUKA FILM EPISODE YA 02 TULIISHIA... "Mamaaaaaa...." Some alikuwa ni kijana wa mjini sana alipiga kelele baada ya kuona sura ya yule mtu imeanza kuoza na meno yake yakiwa na damu mingi. Ghafla jamaa akafumbua macho yake mekunduuuu yaliyo onyesha njaa kali, some akainuka haraka na kutaka kukimbia anavutwa na kurudishwa pale chini. "Aaaaaaaaaa.... " ENDELEA... "aaaaaa...Hapana usiniuwe..." Same alipiga kelele alipoona yule zombi anapeleka mdomo kwenye bega lake Tena akiwa amepanua mdomo wote. ""Ahaaaaaaaaa..." Same aliendelea kupiga kelele lakini yule zombi akaacha haraka na kusimama juu . Same alisimama kwa kasi na kukimbia kuelekea kwenye gari yake simu yake aliacha palepale chini hakuwa na mda nayo. "Hivi kweli nilitaka nimle mtu haiwezekani kwa hiyo mimi zombi?.." aliongea moyoni yule Zombi akiwa anamtazama same kwa mbali akitimua gari yake kwa Kasi Sana. "Alinigonga na gari lakini sijafa Wala sijasikia mau...

PENZI LA KIKOMANDO EPISODE 2

Picha
PENZI LA KIKOMANDO ABELUKA FILM EPISODE:02 TULIISHIA Kiongozi anatoa amri kwa sauti kali "uweniiiiiii" ghafla sauti nyingine ya kike inasikika nyuma yao. "Subirini kwanza ..." Ilikuwa ni sauti nyororo tamu sana iliyowafanya waasi wote wageuke kutazama ni nani huyo aliyefika hapo majira hayo ya usiku ndani ya msitu wa vita? ENDELEA... Waasi wote wanageka na kumuona mwanamke mmoja mrembo aliye shika siraha kubwa mkononi . "We binti ni nani?..na unafanya nini saa hizi za usiku? au upo pamoja na huyu mwanajeshi?...." Aliongea Aboku ambaye ni Kiongozi wa wale waasi taratibu akiwa anamsogelea karibu yule mwanamke. "Naitwa wonder nimekuja kufanya biashara na nyie, ila kama hamtoitaji mi naondoka..? Aliongea binti kwa mapepe sana akiwa anamuangalia James. "Biashara!!, Biashara gani binti?...." Aliuliza Aboku akionekana kushangazwa . Wonder taratibu anaingiza mkono wake kwenye suruali aliyovaa na kutoa kitu ambacho kinamfanya Aboku ashituke na ...

ANGA LA WASHENZI SEHEMU YA 2

Picha
ANGA LA WASHENZI ---- 02 Simulizi za series “Vipi, kaka kuna tatizo?” Mwanamke aliuliza. Alikuwa amevalia suruali ya jeans na tisheti nyeupe ya bia ya Serengeti. Mkono wake wa kuume alikuwa ameshikilia sahani ndefu ya plastiki iliyobebelea kinywaji cha Balimi. . . . “Hamna tatizo dada,” Jona alijibu akipangusa uso. Alinyanyua kinywaji chake akapiga mafundo mawili. Mwanamke alimtazama kwa mashaka. Ni wazi alikuwa anastaajabu kutingwa kule kwa mwanaume huyo. . . . “Samahani,” akasema. “Nilitaka kujua kama utahitaji chochote toka jikoni.” “Ooh, kuna chakula gani?” Jona akauliza akiketi vema kitini. “Nyama ya kukaanga, rosti, ndizi, chips na ugali.” . . . Jona akatazama saa yake ya mkononi. Muda ulikuwa umeenda, na pia alihisi uchovu. Aliona ni vema akabeba chakula moja kwa moja aende nacho nyumbani, hivyo akaagizia na kungoja. . . . Baada ya muda mfupi, chakula kikaletwa, akalipia na kuondoka. Toka hapo bar mpaka nyumbani kwake si mbali. Mwendo wa wastani ungekufikisha kwa takribani dakik...

JOANA ANAONA KITU USIKU SEHEMU YA 2

Picha
JOANA ANAONA KITU USIKU 02 MTUNZI: STEVE MOLLEL Mwanafunzi aliyefariki alijulikana kwa jina la Judith Onenke, mwanafunzi kutoka Nigeria. Miongoni mwa wanafunzi wacheshi na wenye uwezo mkubwa darasani. Masomo yakaihirishwa na taarifa ikatolewa polisi waliokuja mara moja kupeleleza tukio. Walipekua na kuchambua mazingira ya chumba yalipotokea mauaji. Wakamuuliza pia na maswali kadhaa meti wake marehemu Judith, aitwaye Lilian Smith. Ambaye kwa muda wote huo alikuwa anatetemeka kwa hofu na bumbuwazi. Aliona kama tamthilia ya kuigiza inatukia mbele ya macho yake, ila tamthilia asiyoipenda, inayotisha, na rimoti imejamu asiweze kubadili. "Wakati mwenzako anapiga kelele usiku, wewe ulikuwa wapi?" Aliuliza askari. Alikuwa mwanaume mnene mrefu. Mweupe sana. Pua yake ilikuwa nyekundu. Mustachi dhaifu na lips nyembamba. Macho yake yalikuwa madogo ila makali. Alijitambulisha kwa jina la inspekta Bronel Westgate. "Mimi sikusikia lolote," akajibu Lilian akitikisa kichwa. Macho y...

PANIELA (SEASON 1) SEHEMU YA 2

Picha
PANIELA SEASON 1 SEHEMU YA PILI MTUNZI : PATRICK CK ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA Tayari mtuhumiwa amekwisha ingizwa mahakamani na aliyekuwa akisubiriwa ni jaji anayeisikiliza kesi ile aweze kuingia na kuisoma hukumu.Wakati wakimsubiri Jaji aingie,Jason Patrick mwanasheria anayemtetea Penny alikuwa akibadilishana mawili matatu na mteja wake . “ Jason,kabla hukumu haijaanza ninaomba nikwambie kitu.” Akanyamaza kidogo na kuendelea. “ Nakushukuru sana kwa kila kitu ulichonifanyia. Umenisimamia katika kesi hii kwa kila namna ulivyoweza.Naju a chochote kinaweza kikatokea siku ya leo hivyo nakuomba endapo ikitokea nikakutwa na hatia na kufungwa kifungo cha maisha au kifo uhakikishe yale yote niliyokuandikia katika karatasi unayatimiza.Wewe ni zaidi ya rafiki.Wewe ni ndugu yangu pekee ninayekutambua.Ninakukabidhi kila kilicho changu endapo mambo yataenda kinyume na matarajio yetu." Akasema Penny huku machozi yakimtoka “ Penny naomba usikate tamaa hata kidogo.Nimepambana vya kutosha kuhakik...

DIMBWI LA HUBA SEHEMU YA 3

Picha
SIMULIZI: DIMBWI LA HUBA MTUNZI: ALLY MBETU SEHEMU YA TATU “Vipi?” “Safi, pole na kazi.” “Asante, nikusaidie nini?” “Zulfa yupo?” “Zulfa! Wewe nani unayemuuliza Zulfa?” “Ni rafiki yake, naomba uniitie.” “Mmh! Wewe ndiyo uwe rafiki na Zulfa?” yule mtunza nyumba alishtuka. “Ndiyo, naomba uniitie.” “Siwezi, unataka nifukuzwe kazi kwa ajili yako, unamjua Zulfa au unamsikia?” “Huwezi kufuzwa.” “Ndugu yangu, wavulana wengi wamekuwa wasumbufu sana kiasi cha kumfanya mzee ampeleke shule za kukaa hukohuko.” “Najua hunijui lakini Zulfa akisikia nilikuja na wewe umekataa kuonana naye naamini utaikosa kazi na kama utanikutanisha naye nina imani utaongezewa mshahara.” “Wewe umetoka wapi?” “Mjini, najua ana siku chache za kuwepo kabla ya kwenda kusoma nje ya nchi.” “Pamoja na hayo lakini siwezi kukuitia wacha anifukuze kazi kwa kutokuitia muhuni kama wewe.” “Naomba nikutume kitu kimoja wala usimwite atoke nje, nenda tu kamwambie Sued toka mjini yupo nje.” “Halafu?” “Wewe utaona.” “Bwana wewe king’an...

SHAIDA SEHEMU YA 3

Picha
SIMULIZI: SHAIDA MTUNZI: AISHA KHAN SEHEMU YA TATU "Kaelekea wapi? " "Mjini" "Atarudi lini?" "Sijui. aliniambia nimsubiri atakuja kunichukuwa" Mzee Athuman hakuongea zaidi. Alimtazama binti yake na kumsikilitia Kwa kutikisa kichwa kisha akaingia ndani. "Heee!! Sasa itakuwaje mdogo wangu" Shaida aliangua kilio bila kujua nini kitaendelea kwenye Maisha yake. "Usilie, jikaze atakuja kukuchukuwa" "Najikuta naanza kujuta" "Hapana naimani Eddy anakupenda" "Aibu hii sijui ntaipeleka wapi" "Usiongee hivo, kikubwa rudi nyumbani tumsubiri huwenda atakuja hivi karibuni" Aisha alizidi kumtia moyo mdogo wake licha hata yeye pia alikuwa ameanza kupata mashaka. Siku zilisonga Shaida akiwa amerudi kwao. Baada ya mwezi mmoja kupita, dalili za mimba zilianza kujitokeza kwa binti mrembo Shaida. Haikuchukuwa siku mimba iligundulika ikambidi kuvumilia na kuanza kuilea mimba yake akishilikiana na dada yake. M...