Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2022

KOFI LA KISOGO SEHEMU YA 8

Picha
“KOFI LA KISOGO” Na:Arnold Machavo Mbeya—Tanzania Sehemu ipatayo ya 08 ★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★★ ««Ilipokomea... “Kwanini unanikimbia sasa?” Waridi alihoji baada ya kuambiwa ukweli. “Hakuna kitu eti nimefikiria tuu nisogee pembeni,” Zena alimjibu huku akitabasamu. Tabasamu lenye ishara ya kuwa amani ipo kati yao hivyo dada mtu asihofu... TEREMKA NAYO...»» “Sawa hakuna tatizo nashukuru sana kwa msaada wako chei wangu.” “Hahaha eti chei. Hicho kijina chenu na mama nilishakisahau usinikumbushe kabisa hata sikitaki,” Zena aliongea na kusababisha kicheko kwa wote wawili mara baada ya kukumbuka jinsi jina hilo la utani lilivyokuwa likitumika hususani kipindi walipokuwa wadogo. Jioni Hussein aliporejea nyumbani alipokelewa na kitu cha kwanza kwake kilikuwa ni kumuona Hassan wake furaha yake kubwa. Walipotulia Waridi ndiye alikuwa wa kwanza kugusia juu ya kutaka kuondoka kwa Zena. “Haa kwanini sasa? maan...” Hussein aliongea. “Aah aah jamani kaumri kanasogea na yeye,” Waridi alimjibu kwa kumkatis...

UKWELI WENYE KUUMA (PAINFUL TRUTH) SEHEMU YA 70

Picha
Simulizi: UKWELI WENYE KUUMA (PAINFUL TRUTH) Muandishi: NYEMO CHILONGANI SEHEMU YA 70 Mikakati kabambe ikaandaliwa, vijana nane wakatafutwa, vijana ambao hawakuwa na hata na chembe yoyote ya woga, vijana ambao walikuwa na uzoefu mkubwa wa kutumia bunduki wakati wowote na sehemu yoyote bila kuogopa kitu chochote kile. Vijana nane tayari walikuwa wamekamilika na kitu ambacho kilifanyika ni kuanza kusafiri kuelekea Tanzania. Kwa kuwa walitumia usafiri wa ndege ya kukodi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Bwana Dawson wala hawakutumia muda mrefu angani wakawa wamekwishafika Tanzania. Walichokifanya mahali hapo ni kuchukua vyumba katika hoteli ya The Cape na kisha kupumzika. Usiku hawakulala, kitu ambacho walikuwa wakikifanya ni kukusanyika katika chumba kimoja na kuanza kupanga mipango juu ya namna ya kumchukua Andy na kuanza kurudi nae nchini Marekani. Nchi ya Tanzania wala haikuwaogopesha hata kidogo kwani kwao waliuona ulinzi wa nchi hiyo kuwa ndogo sana na hivyo kuwapa nafasi kubwa sana ya ...

MCHUNGAJI MCHAWI EPISODE:25

Picha
Story: MCHUNGAJI MCHAWI Mtunzi: Nellove 😎 Episode: 25 Ilipoishia... Waganga walishindwa kumpindua, wachawi wenzake hawakumfikia na hata baadhi ya wachungaji waliishia kwenye udongo mara tu walipoamua kupambana naye, hata hivyo habari za ujio wa mchungaji Joshua kutoka Morogoro alizipata na siku hiyo alishuhudia watu wakichomolewa mapepo na uchawi aliopanda ndani ya watu hao,,, alishuhudia hayo kwani naye alikuwa katikati ya umati ule kwa lengo maalumu. Mzee Shirima alianza kumjaribu jaribu Mchungaji Joshua. Songa nayo... Mchungaji alipata kuhisi uwepo wa jaribu kutoka kwa mtu mbaya lakini hakutaka kushughulika naye sana,,, aliendelea na shughuli ya kiroho. Hata hivyo utofauti mkubwa ulipata kudhihirika,, Mzee Shirima aliona moto uliosababisha ugumu katika jaribio lake. Hii ilikuwa tofauti na wachungaji wengine kwani pindi alipowajaribu tu alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana. Ile nguvu aliyotuma kumjaribu mchungaji Joshua aliishuhudia ikiteketea na kuyeyuka ndipo aliona ni heri aweke ma...

MSITU WA AJABU EPISODE:66

Picha
Story: MSITU WA AJABU Episode:66 Mtunzi:Nellove Ilipoishia... Alipomaliza kufunga alikirudisha kwenye begi na kuchukua kingine maana walikuwa navyo vingi. Alirudia kauli yake. "Kuna kitu kinachanganya nashindwa kuelewa" "Ni kitu gani?" Aliuliza Joram lakini hata kabla ya kujibu Sylvestre alianguka chini huku damu zikimtoka puani na kwenye masikio. Wote walishituka na kumgeukia hata hivyo hazikupita dakika nyingi naye Daniel alianguka. Songa nayo... Butwaa iliwapiga wote kwa sababu ya hiki kilichotokea. Sylvestre pamoja na Daniel wote walikuwa chini na kadri sekunde zilivyosogea mbele hali zao zilionekana kutokuwa sawa kabisa. Wale wengine wakiongozwa na Mr Tommy walifanya haraka na kumsogelea mwenzao. Ambacho Kilifanyika hapo ni kuchukua baadhi ya vifaa vilivyokuwa ndani ya begi na kuanza kufanya mambo waliyoyajua wao wenyewe katika kuhakikisha mwenzao anakuwa sawa. Wote walimsogelea Sylvestre wakati huo Daniel aliachwa peke yake bila msaada wowote. Hali yake iliend...

Mbeya City Yaichimba Mkwara Yanga

Picha
KOCHA Mkuu wa  Mbeya City, Mathias Lule, ameitahadharisha Yanga, kuwa isitarajie kupata mteremko katika mchezo ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, watakapokutana Februari 5 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.   Mbeya City, wapo nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara wakiwa na pointi 22 kibindoni  huku wakiwa  wameshuka uwanjani mara 13 wakiwa juu ya Azam FC kwa pointi moja malengo yao mwakani ni kushiriki michuano ya Shirikisho barani Afrika.   Lule amesema kuwa malengo yao ni kucheza michuano ya Shirikisho mwakani ili kuwapa uzoefu wa michuano ya kimataifa wachezaji wake kama ilivyokuwa kwa Namungo na Biashara ambazo kwa misimu ya karibuni zimeiwakilisha nchi pamoja na Simba.   “Tunapaswa kuwa na muendelezo mzuri katika michezo minne ijayo ili kujiwekea katika mazingira mazuri yakutimiza malengo yetu ambayo yatatimia kama tutapata ushindi kwenye michezo yetu,”  alisema Lule.   Mbeya City watakuwa kibaruani Februari 5, kuwakab...

Mo Salah Aizamisha Morocco, Aipeleka Misri Nusu Fainali

Picha
Mshambuliaji wa Liverpool, Mohamed Salah ameiongoza Egypt kwa mara nyingine kuhakikisha wanatinga hatua ya nusu Fainali. Katika mchezo huo Mafarao hao wa Misri walitoka nyuma na kuibuka na ushindi wa Magoli 2-1 baada ya muda wa nyongeza.   Morocco ndio waliokuwa wa kwanza kupata goli kwa mkwaju wa penati uliowekwa kimiani na S. Boufal dakika ya 7 ya mchezo.   Morocco walikwenda mapumziko wakiwa kifua mbele lakini kipindi cha pili Mafarao wa Misri walikuja kivingine na Mohamed Salah aliwasawazishia Misri dakika ya 53 na kufanya mchezo huo kumalizika kwa sare ya goli 1-1.   Mchezo uliongezwa dakika 30, ambapo Salah kwa mara nyingine akatoa pasi ya goli la ushindi kwa Trezeguet dakika ya 100. Egypt inakwenda kukutana na mwenyeji wa michuano hiyo, Cameroon katika mchezo wa nusu Fainali.

Greenwood Akamatwa kwa Tuhuma za Ubakaji

Picha
Mchezaji wa Manchester United Mason Greenwood amekamatwa kwa tuhuma za ubakaji na shambulio kufuatia madai kwenye mitandao ya kijamii.   Polisi wa Greater Manchester walisema ilifahamishwa kuhusu “picha na video za mitandao ya kijamii zilizotumwa na mwanamke akiripoti matukio ya unyansaji wa kingono”.   Iliongeza “tunaweza kuthibitisha kuwa mwanamume mwenye umri wa miaka 20 amekamatwa kwa tuhuma za ubakaji na shambulio”.   Anaendelea kuzuiliwa kwa mahojiano na uchunguzi unaendelea. Manchester United hapo awali ilisema mchezaji huyo hatarejea kwenye mazoezi au mechi hadi ilani nyingine.   Klabu hiyo ilisema “haikubaliani na vurugu za aina yoyote” na imefahamishwa kuhusu madai hayo kwenye mitandao ya kijamii lakini haitatoa maoni yoyote zaidi hadi “ukweli utakapothibitishwa”.   Greenwood hajajibu madai hayo ya mitandao ya kijamii. Greenwood mwenye umri wa miaka 20, ambaye aliichezea klabu hiyo kwa mara ya kwanza Machi 2019, alisaini mkataba w...

TP Mazembe Wamfuata Msuva Dar

Picha
UONGOZI wa Klabu ya TP Mazembe, umefunguka kuhitaji kumsajili winga Mtanzania, Simon Msuva anayekipiga Wydad Casablanca ya Morocco, huku ukiweka wazi mipango yao ya kuhitaji kukirudisha kikosi chao katika mafanikioya kimataifa kunako michuano ya Afrika. Msuva licha ya timu yake ya Wydad Casablanca kuendelea kucheza katika mashindano mbalimbali, lakini winga huyo yupo Tanzania akiendelea kujifua, huku ikielezwa kwa sasa hayupo kwenye maelewano mazuri na mabosi wake hao kutoka Morocco.   Bosi mmoja kutoka TP Mazembe ambaye hakutaka kutajwa jina lake, ameliambia Spoti Xtra kwamba, wapo kwenye mikakati ya kuhitaji kumsajili Msuva, huku akisema malengo yao ni kuja hapa nchini kwa ajili ya kufanya mazungumzo na muhusika ambaye wanaamini kama watamsajili basi atawasaidia hususan katika michuano ya kimataifa. “Ni kweli Msuva ni moja kati ya wachezaji ambao tumekuwa tukiwahitaji kwa muda mrefu kabla hajajiunga na Wydad Casablanca, lakini shida kubwa kwa kuwa alikuwa anachez...

BEYOND LOVE (ZAIDI YA MAPENZI) SEHEMU YA 1

Picha
SIMULIZI: BEYOND LOVE (ZAIDI YA MAPENZI) SEHEMU YA 1 Tom aliheshimika na kutisha, hakuna mtu aliyechezea shughuli zake kutokana na uhusiano mzuri aliokuwa nao na viongozi Serikalini, akiwa mdhamini wa Chama Tawala. Hakuna mtu ambaye hakumfahamu, kila alipopita watu walionyeshana vidole, alikuwa na marafiki wengi kupita kiasi. Ilipotokea akaa peke yake kwenye baa au hotelini, ndani ya dakika mbili tayari alishazungukwa na watu, kila mtu akiagiza alichotaka kutumia, kwa Tom kulipa haikuwa tatizo, fedha alikuwa nayo. Tabia hii ilimfanya awe na wapambe wengi kila alikokwenda, akilindwa na watu ambao wala hakuwapa kazi hiyo. Hayo ndiyo yaliwahi kuwa maisha ya Tom, lakini vitu vyote hivyo havikuwepo tena, vilikuwa vimeyeyuka na yeye kujikuta amelala kitandani kwa miaka mitano bila kuwa na fahamu, akiwa amepooza mwili wote isipokuwa kichwa tu! Marafiki wote aliokuwa nao walimkimbia, mwanzoni kila mtu alifikiri angekufa wiki ya kwanza lakini akaendelea kuwepo mpaka mwaka ukaisha, ukaja wa pili...

KIJIJINI KWA BIBI SEHEMU YA 6

Picha
RIWAYA : KIJIJINI KWA BIBI. MTUNZI : ALEX KILEO. SEHEMU YA SITA. _______________ ILIPOISHIA.. ________________ Omari alipotoka msalani akawa anaelekea nje kuwafuata wenzake, ndipo mbele yake akawaona Askari wapatao watano wakiwa wanaelekea upande aliopo huku wameongozana na msichana ambae hakuweza kumtambua kutokana na umbali ulikuwa kati yao, ila kadri walivyozidi kusogeleana ndipo sura ya yule msichana ilivyozidi kumjia, zilipofika hatua mbili kabla hawajapishana ndipo Omary alipopata mshtuko baada ya kugundua kuwa yule msichana ni Mhudumu wa ile bar ambayo Kayoza alifanya mauaji. Omary aliuficha mshtuko wake ila sasa yule Mhudumu akawa anamuangalia sana Omary, Omary akatamani hata apotee gha fla kama upepo ila i l ishindikana na akaamua aendelee tĂș kwenda mbele kiume. Wale Askari na mhudumu walipomfikia Omary wakampita na kufanya Omary ashukuru Mungu baada ya kupishana nao. Yule Mhudumu alipompita Omary, alihisi hiyo sura siyo ngeni kwake, alitembea hatua mbili kisha akasimama, ikab...

ASANTE KWA KUNIFUTA MACHOZI (HISIA ZANGU) SEHEMU YA 13-14

Picha
Simulizi: ASANTE KWA KUNIFUTA MACHOZI (HISIA ZANGU) Mwandishi: JOSEPH SHALUWA SEHEMU YA 13 Nimejiuliza maswali mengi lakini bado sijapata majibu. Kweli Lilian umesahau mapema kiasi hicho? Kweli umesahau wema wangu wote? Sasa naanza kuamini kuwa, kumbe hukuwa na mapenzi ya dhati kwangu. Nimeelewa ni kwanini ulikuwa unaninyima penzi lako. Bila shaka utakuwa umeshatolewa bikra ndio maana hukutaka nijue. Umeniumiza sana. Nahisi harufu ya damu mbichi ndani ya moyo wangu. Hata hivyo, bado una nafasi ya kutafakari upya. Una muda wa kufikiri na kuamua vinginevyo kama utaona inafaa. Nakupenda sana kutoka ndani ya moyo wangu. Ahsante kwa yote lakini kumbuka sikupaswa kuachwa kwenye maumivu makali kiasi hiki, tena wakati huu wa mwanzoni kabisa wa masomo yangu huku Malaysia. Moyo wangu unateseka! Edo. Kwa hakika Edo hakuweza kuvumilia, muda wote aliokuwa akiandika ujumbe ule, machozi yalikuwa yakimtiririka mashavuni mwake. Haikuwa rahisi kukubaliana na hali ile. Hakuweza kufanya chochote tena, baa...

AKWELINA SEHEMU YA 9

Picha
AKWELINA SEHEMU YA 9 Wanaume hao wakamnyanganya mtoto Monna alafu wakamuweka chini kisha wakamshika Monna wakamlaza chini wakamvua nguo, Kiongozi wao akasimama akafungua zipu ya suruali yake alafu akajiandaa kumuingilia Monna , Kiongozi wa vijana hao kabla hajamfikia Monna walisikia mngurumo wa gari, wakamziba mdomo Monna wakaingia nae ndani ya Pango wakamthibiti Monna vizuri, Gari lililofika eneo hilo lilikuwa limembeba Kakinga , Kakinga aliposhuka toka kwenye gari alianza kumwita Monna kwa sauti ya juu sana , Kakinga aliita kwa hisia na machungu makali lakini kimya kilizidi kutawala eneo hilo . Kakinga alizidi kumwita Monna bila kuchoka kakinga alizunguka eneo kubwa katika eneo hilo la kutupia uchafu ( Jalalani ) bila mafanikio, wakati huo Monna alikuwa anamuona na anamsikia mume wake lakini hakuweza kumjibu kutokana na kuzibwa mdomo, Muda ulizidi kwenda Dereva aliyemsaidia kakinga alimfuata Kakinga akamwambia: DEREVA: Tuondoke Kaka muda unazidi kwenda alafu hili gari sio langu kwahi...

MISS TANZANIA SEHEMU YA 15

Picha
MISS TANZANIA SEHEMU YA 15 MTUNZI : PATRICK.CK ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA .Akaufungua na kuusoma huku moyo wake ukienda kwa kasi sana..Ujumbe ule ulitoka kwa Margreth Kibaho ‘Kesho saa nne asubuhi Sean snacks Mbezi.margreth” baada ya kuusoma ujumbe ule akaufuta kabisa katika simu yake. ENDELEA........................ Saa kumi na moja alfajiri Vero ndiye aliyekuwa wa kwanza kuamka .Hakutaka kumwamsha Patrick.Taratibu akaingia bafuni akaoga kisha akavaa nguo na kumwamsha Patrick. “Patrick naondoka” Patrick akafikicha macho yaliyojaa usingizi akasema “Mbona mapema hivyo kuna nini? “Nothing.Tutaonana” Ni wazi Veronika aliondoka akiwa bado na hasira na haikuhitaji akili ya ziada kung’amua kuwa dada huyu mrembo alikuwa amekasirika.Patrick hakutaka kujibizana naye ingawa aliumia sana moyoni kwa hali ile waliyoifikia katika uhusiano wao. Akiwa hapo kitandani Patrick akajaribu kurudisha kumbukumbu nyuma toka walivyoanza kufahamiana na Happy ,urafiki wao ulivyoanza hadi walivyokuja kutengana.K...