MISS TANZANIA SEHEMU YA 15



MISS TANZANIA

SEHEMU YA 15

MTUNZI : PATRICK.CK

ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA

.Akaufungua na kuusoma huku moyo wake ukienda kwa kasi sana..Ujumbe ule ulitoka kwa Margreth Kibaho
‘Kesho saa nne asubuhi Sean snacks Mbezi.margreth”
baada ya kuusoma ujumbe ule akaufuta kabisa katika simu yake.

ENDELEA........................

Saa kumi na moja alfajiri Vero ndiye aliyekuwa wa kwanza kuamka .Hakutaka kumwamsha Patrick.Taratibu akaingia bafuni akaoga kisha akavaa nguo na kumwamsha Patrick.
“Patrick naondoka”
Patrick akafikicha macho yaliyojaa usingizi akasema
“Mbona mapema hivyo kuna nini?
“Nothing.Tutaonana”
Ni wazi Veronika aliondoka akiwa bado na hasira na haikuhitaji akili ya ziada kung’amua kuwa dada huyu mrembo alikuwa amekasirika.Patrick hakutaka kujibizana naye ingawa aliumia sana moyoni kwa hali ile waliyoifikia katika uhusiano wao.
Akiwa hapo kitandani Patrick akajaribu kurudisha kumbukumbu nyuma toka walivyoanza kufahamiana na Happy ,urafiki wao ulivyoanza hadi walivyokuja kutengana.Kumbukumbu zikamjia siku alipoiona suya ya Happy katika Luninga na akapoteza fahamu.Kumbukumbu zikamrudisha tena Diamond Jubilee ambako Happy alitwaa taji la miss Tanzania.
“Ni lazima nionane na Happy .”Alitamka maneno haya kwa sauti.
Taratibu akajiinua kitandani na kuingia bafuni kujimwagia maji.Akiwa chumbani kwake akijiandaa mara simu yake inaita.Ilikuwa ni simu toka kwa mama yake.
“Sikamoo mama ‘
“marahaba.Hivi wewe mtoto una matatizo gani jamani?Umepatwa na nini Patrick?Hivi ni kitu gani kinakusumbua we mtoto? Mama yake alisema kwa ukali.mama huyu ni mmoja kati ya akina mama wakali na asiyependa mchezo
“mama kwani kuna nini mbona hivyo? Aliuliza Patrick makusudi hali akijua kuwa amekwisha likoroga.Alijua tu tayari Vero atakuwa amekwenda kushtaki nyumbani .
“Umemfanya nini mwenzio?
“nani Vero?
“sasa kwani una wenzio wangapi?
“hakuna chochote kibaya mama nilichokifanya .Ni tatizo la kupishana kauli tu”
“sasa sikiliza Patrick nataka ufike hapa nyumbani haraka sana asubuhi hii.Mbona unaanza kutuumiza vichwa we mtoto?Alifoka mama yake
Patrick hakujibu kitu akakaa kimya kwa sekunde kadhaa kisha akastuliwa tena
“Umenisikia lakini?Nataka uje hapa nyumbani haraka iwezekanavyo.Na ukae ukijua kuwa kesho ni lazima usafiri vinginevyo umtafute mama yako.”
Patrick kijasho kikamtoka.Akajikaza na kusema
“mama huko unakofika sasa ni mbali mama yangu.Nitakuja nyumbani tuongee ila si kwa asubuhi hii.Kuna mahala natakiwa niende Nina miadi ya muhimu sana “
“Hiyo miadi ni muhimu kushinda wito wangu mimi mama yako?
“Nothing is important than you mother”Akajibu Patrick
“Ah! Ah! Ah!!! Sitaki kabisa kusikia hivyo vingereza vyako.Kama unaona mimi ni muhimu njoo nyumbani haraka sana.”
“mama samahani siwezi kuja nyumbani sasa hivi .Tayari nina miadi na mtu na ananisubiri asubuhi hii .Nitakuja baada ya kutoka huko.M…..
Kabla hajaendelea akasikia simu ikikatwa.Patrick akabaki njia panda.Je aende kwa mama yake au aende katika miadi yake na Margreth?
Akiwa amezama katika fikra nzito hajui nini cha kufanya mara mlango unagongwa na Andrew akaingia.
“Hi Patrick” Andrew akasema
“Hi” Patrick akajibu
“Hebu niambie ndugu yangu mambo yanakwendaje kwa sababu nimepokea simu toka kwa mama asubuhi hii akilalamika sana juu yako.Anasema kuwa Vero ameenda pale alfajiri na kumweleza kuwa umebadilika mno kwa siku hizi za karibuni.Na kikubwa zaidi ni kukataa safari ya kwenda London.Hilo ndilo linawafanya wawe na hasira juu yako.Sikiliza Patrick kuna kitu kimoja ulichokosea nacho ni kuonyesha wazi wazi kuwa kuna jambo zito linakusumbua.Tayari Vero amekwisha ng’amua hilo .Na hili la kukataa kwenda safari ndio limedhihirisha wazi kuwa kuna kitu unakificha.Chonde chonde Patrick jaribu kuwa makini ili tusije haribu mambo.”
Patrick akafikiri kidogo kisha akasema
“ Andrew nakubali nilifanya kosa kuonyesha wazi wazi kuwa kuna suala linanisumbua.Nilishindwa kujizuia.That was a mistake.Lakini hata iweje safari hiyo ya kwenda shopping Uingereza siwezi kwenda.Leo nina miadi na Margreth na ninafikiri baada ya hapo nitaonana na Happy sasa huoni kuwa kwenda kwangu London kutaharibu kabisa mpango wangu mzima wa kuonana na Happy .Ni wazi ninahitaji kuonana na Happy .”
“lakini Patrick mimi bado kuna kitu kimoja ninakifikiria ambacho kinaniumiza kichwa sana” Andrew akasema
“Jambo gani hilo” Patrick akauliza huku akimkazia macho Andrew
“Kuhusu wazazi wako pindi watakapokuja gundua kuwa unampango wa kuonana na Happy ”
Patrick akatabasamu kidogo halafu akasema
“Andrew masuala haya yote niachie mimi”
“Siwezi kukuachia wewe peke yako Patrick kwa sababu mimi na wewe tunaonekana ni kitu kimoja.Chochote unachofanya wanajua na mimi nimeshiriki.Ukikosea wewe na mimi nimekosea pia.”
“Kwa hiyo unataka kusemaje Andrew? Patrick akauliza
“ Nafikiria kitu kimoja”
“Kitu gani hicho?
“Naona ni bora tu angali bado mapema uachane na suala hili la Happy .Kwa sasa uko katika maandalizi ya kumuoa Vero , huoni kuwa kuendelea kulipa kipaumbele suala hili la kuonana na Happy linapelekea hata masuala mengine ya msingi kuhusu ndoa yako kuanza kuharibika?.Naona ni bora ukaelekeza nguvu zako katika suala la ndoa yako.Suala la Happy bado halina uzito sana kwa sasa Isitoshe imekwisha pita miaka mingi na tayari Happy ana mchumba wake.Sioni sababu ya kutumia nguvu nyingi katika kumtafuta mtu ambaye alikutia matatizoni halafu baade akakuacha na kwenda zake Ulaya.Vero ndiye mwanamke pekee aliyekaa nawe katika kipindi chote hiki cha matatizo na ambaye amesimama na wewe hadi sasa ambapo maisha yako tayari yamekaa sawa.Hivi unavyofanya si vizuri na ninakwambia ukweli rafiki yangu unamuumiza Vero sana.” Andrew akasema na kumtazama Patrick usoni ambaye maneno yale yanamfanya abadilike uso wake.
“What the hell are you talking about Andrew?. Patrick akauliza kwa ukali.
“Andrew nimekwisha kwambia mara nyingi kwamba kama hutaki kuwa upande wangu naomba uniache.Sikulazimishi kushiriki katika masuala yangu”
“Patrick ! huo ulikuwa ni ushauri wangu tu na si lazima uufuate.Pamoja na ushauri huo niliokupa kama rafiki yako,lakini mwisho wa siku mwenye uamuzi juu ya masuala yako ni wewe mwenyewe..Ok tufanye kama unavyotaka”

************************

Saa nne kamili juu ya alama ilimkuta Patrick katika maeneo ya Sean snacks.Hakutaka kupoteza hata dakika moja katika miadi hii ya muhimu.Sehemu hii ni moja kati ya sehemu tulivu sana .Ni mahali panapofaa sana hasa kwa maongezi ya faragha.
Mara tu aliposhuka garini alitumia muda wa kama dakika kumi kuzunguka maeneo hayo kwa minajili ya kuangalia kama anaweza akamuona Margreth.Mara simu yake ikalia.Zilikuwa ni namba ngeni.
“Halloo “ Patrick akaita
“Margreth hapa uko wapi Patrick?
‘Nimeshafika kitambo ,nilikuwa najaribu kuangaza angaza kama nitakuona”
“Mimi ndio nafika sasa hivi.Njoo basi huku nyuma kiunga L”
Akiwa bado amesimama alijikagua kwanza na kuhakikisha yuko katika muonekano nadhifu kisha akapiga hatua kuelekea mahala alikoelekezwa.
“Wow Patrick” Ilikuwa ni sauti ya Margreth mara tu alipomuona Patrick.Patrick hakusema kitu akamtazama Margreth kisha akamkumbatia kwa nguvu.Margreth machozi yalikuwa yakimtoka.Mtu aliyesemekana kufariki dunia leo hii wameonana.
“Patrck siamini kama leo tumekutana tena.Siamini kwa kweli” Margreth akasema huku akifuta machozi.
“Patrick sitaki kulia tena .Tumekwisha lia vya kutosha kwa ajili yako.Tunashukuru Mungu kwamba u mzima na ametukutanisha tena.Huu ni kama muujiza ambao hakuna aliyeutegemea.” Margreth akasema
“sawa kabisa Margreth hata mimi sikutegemea kabisa kama nitakuja kuonana nanyi tena hasa kutokana na mambo yaliyotokea .Na ndio maana nilipatwa na mstuko wa moyo baada ya kumuona tena Happy katika Tv .Hebu kabla hatujaendelea naomba unipe japo kwa muhtasari maendeleo ya hali ya Happy .”
“Happy anaendelea vizuri” Margreth akasema kwa ufupi huku akimtazama Patrick usoni kwa makini.
“Really?
“Yes .She’s fine.Tuachane na hayo.tuendelee na kilichotukutanisha hapa” Margreth akasema
“Ok Margreth ,lakini naona tumejisahau hata kuagiza vinywaji.Sijui unatumia nini?
“Mimi nakunywa wine.Wewe je bado unaendelea na kunywa Juice mpaka sasa?
“Yes margreth.Patrick habadiliki.Umuonaye ndiye Patrick yule yule wa zamani..Ingawa mhh mwenzangu umebadilika sana yaani umependeza sasa hivi umekuwa msichana mrembo kama dada yako Happy .” Wote wakacheka kisha Patrick akainuka na kufuata vinywaji.
“Patick” Alianza maongezi Margreth baada ya Patrick kurejea na vinywaji.
“Ni mengi sana yametokea katika kipindi hiki tulichopotezana.Ni mambo mengi kiasi kwamba tukianza kukumbushana itachukua siku nzima.Kabla sijaendelea kwa niaba ya familia yetu nakupa pole nyingi sana kwa yote yaliyotokea.Sitaki kukumbusha mateso na machungu ya adhabu ile ya kifungo lakini kwa dhati kabisa naomba niweke wazi kuwa familia yetu haikukutupa na kukuacha peke yako gerezani.Baada ya Happy kuondoka alituachia jukumu la kukuangalia mara kwa mara gerezani.lakini baadae zikaja taarifa kuwa umehamishwa gereza na ndio wakati huo huo baba akawa amestaafu kazi tukahama Mbeya na kuhamia Dar es salaam.Toka hapo ndipo utengano ulipoanzia.Tulipofika Dar mdogo wetu akaanza kuumwa hivyo tukatumia muda mwingi kumuuguza kiasi cha kukusahau kabisa.Kitendo hiki cha kukusahau tayari kimetia doa kubwa sana baina yako na sisi.”
Akanyamaza akanywa funda kadhaa za wine kisha akaendelea.
“Patrick kitu kingine kilichotufanya tukate tama kabisa ni baada ya kupata taarifa kuwa umefariki ukiwa gerezani”
“Nimefariki nikiwa gerezani ? Patrick akauliza kwa mstuko.
“Yes Patrick Happy alipata taarifa kwamba umefariki ukiwa gerezani.”
Patrick akavuta pumzi ndefu halafu akaseam kwa sauti ndogo
“I cant believe this.Nani alimtumia taarifa hizo kwamba nimefariki dunia?
“Siwezi kufahamu Patrick taarifa za kifo chako alizipata toka kwa nani.Suala hilo atakueleza yeye mwenyewe kwa kirefu pindi mkionana uso kwa uso” Margreth akasema
Patrick akazama katika mawazo mengi ya ghafla.taarifa ile ya kwamba alikuwa amefariki dunia ilikuwa imemstua mno.
Margreth akamtazama Patrick usoni halafu akaendelea.
“ Ni vigumu mno kulezea uchungu uliotupata baada ya kupata taarifa ile.Happy alilia mno ,akawa akizimia kila siku mpaka ikabidi baba na mama wasafiri kwenda marekani kukaa naye na kumfariji.Baada ya kumaliza masomo yake Happy alirudi nyumbani na kitu cha kwanza alichokifanya ilikuwa ni kutafuta ni wapi ulikozikwa.Baada ya kufanya uchunguzi ikagundulika kuwa taarifa zile za wewe kufariki hazikuwa za kweli.Tulikaa tukimuomba Mungu kwa mapenzi yake atukutanishe siku moja.Mungu amesikia maombi yetu na hatimaye leo hii tumeonana.”
Margreth akatulia ,akachukua glasi yake ya wine na kupiga funda kadhaa.Patrick jasho lilikuwa likimtoka.Alikosa kitu cha kuongea.Kutokana na joto kali alilokuwa akilisikia akavua koti kisha akatoa kitambaa na kujifuta jasho lililokuwa likimtiririka kwa wingi.Machozi yalimlenga lenga.
“Patrick” Margreth akamstua
“Haikuwa dhamira yangu kuongea mambo haya ila ni katika kuweka mambo na kumbukumbu sawa. kikubwa kilichonifanya nikutafute kwa hali na mali ni suala hili lililoko mbele yetu.Patrick suala hili ni suala gumu sana.kwa taarifa yako ni kwamba Happy alipatwa na mstuko mkubwa mpaka akapoteza fahamu mara tu alipokuona.Leo hii umeniambia kuwa hata wewe ulipatwa na mstuko baada ya kumuona Happy katika Tv na wewe ukapoteza fahamu.Happy kwa sasa yuko katika wakati mgumu sana akitafuta jinsi ya kuonana na wewe na nina imani hata wewe pamoja na yote yaliyotokea utakuwa na shauku ya kutaka kuonana na Happy .”
Margreth akanyamaza na kimya kikapita.
“Patrick hali ya Happy si nzuri.Nasema si nzuri kimwili na hata kiakili.Tangu amekuona Diamond Jubilee Happy anashindwa hata kula.anashinda analia.Hakuna mwingine anayetaka kuongea naye zaidi yangu.Mimi peke yangu ndiye inayeweza kuongea naye tukaelewana.Ni kutokana na hali yake hii imenibidi nichukue jukumu la kukutafuta ili tuone ni jinsi gani tunaweza kulitatua tatizo hii lililoko mbele yetu.Pamoja na kwamba mmepotezana miaka mingi sasa lakini nina imani wakati mnapotezana kila mmoja alikuwa bado akimhitaji mwenzake na ndio maana baada ya kuonana kila mmoja amepatwa na mstuko wa ajabu.Kitu ninachohitaji kukifanya ni ninyi kukutana .”
Margreth akakaa kimya na kuyaacha maneno yale yazame kabisa ndani mwa Patrick.
“Yes ni lazima mkutane tena.Kinachomuumiza Happy kwa sasa ni jinsi gani atakavyoweza kuonana na wewe.Nina imani hata wewe utakuwa na hamu ya kuonana na Happy japokuwa miaka imeenda na kila mmoja kwa sasa ameendlea na maisha yake.Nina imani mtakapoonana mtaongea na yatakwisha.najua kila mmoja analo la kumweleza au kumuuliza mwenzake kwa hiyo mtakapokutana utakuwa ni mwanzo mpya wenye amani.Hata kama hamtarudiana tena lakini litakuwa jambo jema kama mtamaliza tofauti na kuendelea kuishi kwa amani.”
Patrick alikuwa kimya kabisa jasho likiendelea kumtiririka.Akarekebisha koo na kusema
“margreth uko sahihi.Ni lazima nionane na Happy .”
Margreth akatabasamu kisha akasema.
‘Ok Patrick nashukuru sana kama umeridhia kuonana na Happy .Nimefurahi sana.Nina imani ni fursa hiyo ambayo hata Happy alikuwa akiingojea kwa hamu kubwa.Sasa basi kama unavyojua Happy kwa sasa ni mrembo wa Tanzania.Tayari ana jina kubwa.Kila analolifanya yeye kwa sasa linakuwa ni habari.Vyombo vya habari na hasa haya magazeti ya udaku yanamfuatilia usiku na mchana.Kwa hiyo basi hatutaki kutengeneza story na kuwafaidisha watu.Makutano haya yawe ni ya siri kubwa kiasi kwamba iwe ni siri baina ya mimi wewe na Happy .makutano yenu yafanyike nje ya dare s salaam ambako hamjulikani kabisa.Mimi napendekeza makutano yenu yawe morogoro au we unasemaje?
Patrick akafikiri kisha akasema
“Hapana margreth Morogoro bado ni karibu sana na Dar es salaam.Morogoro hapawazuii watu kufunga safari na kuwafuatilia hasa wakijua kuwa wanatengeneza story ambayo itawaingizia fedha.Mimi napendekeza tukakutanie Arusha.Tena nje kabisa ya mji.Pale tunaweza kukaa tukaongea na kuweka mambo sawa bila kuingiliwa na mtu yeyote yule.Au we unaonaje margreth?
“Hilo ni wazo zuri .Tena zuri sana.Nina imani hata Happy mwenyewe hawezi kulipinga kwa sababu akili yake yote kwa sasa ni kuonana na wewe tu hata kama makutano ni Ulaya.Ok hebu nipe dakika tano hivi niongee naye nisikie anasemaje.”
“Ok Margreth.”
Margreth akatoa simu yake na kwenda mbali kidogo na mahali walipokuwa wamekaa akapiga simu.
Baada ya kama dakika kumi hivi akarejea.
“Enhee anasemaje Happy ? Patrick akauliza kwa shauku.
Huku akitabasamu Margreth akajibu
“Amekubali bila wasi wasi na tena amefurahi sana yaani bado haamini kama ni kweli”
“wow ! nipe basi niongee naye mimi mwenyewe”Patrick akasema
“No huwezi ongea naye kwa sasa.Mtaongea mkionana uso kwa uso.Kinachotakiwa kwa sasa tupange kabisa utaratibu wa safari ni lini na ni wapi mtakwenda kukutana,nina maana ni hoteli gani mtafikia.”
Huku akichezesha mguu wake kwa furaha Patrick akasema
“ Kuna hoteli moja mpya kabisa imefunguliwa nje kidogo ya Usa river.Ni sehemu ya kisasa na yenye utulivu wa pekee.Ninadhani inafaa sana kwani hakuna mtu atakayekuja kufuata umbea kule.Kuhusu usafiri gharama zote zitakuwa juu yangu.Wala usihofu.Community airlines wana ndege ya kwenda kaskazini kila siku saa saba na saa kumi na moja jioni.Mimi nitatangulia na ndege ya saa saba mchana na Happy itambidi aje na ndege ya saa kumi na moja jioni.Kwa hali ilivyo hatuwezi kusafiri na ndege moja.Ngoja nimpigie simu rafiki yangu Andrew afanye mpango wa tiketi hizo haraka sana.Usihofu huyu ni zaidi ya rafiki ninamwamini sana.”
Patrick akaitoa simu yake na kumpigia Andrew.
“Haloo Andrew”
“Patrick vipi? Mambo yanakwendaje?
“mambo shwari tu Andrew”
“Sasa Andrew ni hivi,natakiwa niende Arusha leo.hapa niko na Margreth .Nimeongea naye na mwisho wa yote natakiwa nikutane na Happy Arusha.Naomba basi ufanye hima uende pale katika ofisi za community airlines na unifanyie mpango wa tiketi mbili .Ya kwangu mimi ni ya ndege ya saa saba mchana huu na nyingine ni ya Happy Kibaho ndege ya saa kumi na moja.Please Andrew its urgent.”
“Ok Patrick tena imekuwa vizuri kwa sababu hapa nilipo sasa si mbali na ofisi zao ngoja niwahi basi.Nipe kama dakika ishirini hivi nitakupigia simu.
“Ok Andrew”
Patrick akakata simu na kupumua kwa nguvu
“Everything is going to be fine.Hatimaye baada ya muda mrefu ninaenda tena kuonana tena na lulu ya thamani kubwa maishani .” Patrick alikuwa akiongea mwenyewe na kumfanya margreth atabasamu .
Waliendelea kuongea maongezi ya hapa na pale mara simu ya Patrick inalia.
“Ni Andtrew huyu”Patrick akasema
“Haloo Andrew hebu nipe habari”
“Patrick kila kitu tayari.Kuna rafiki yangu yule bwana Kimaro anafanya kazi pale pale amenisaidia sana kufanikisha zoezi hili kwa haraka.Kwa hiyo unaweza kupita ofisini kwangu kwani ndiko naelekea kwa sasa”
“Ok Ahsante sana Andrew nitafika hapo muda si mrefu”
Patrick akakata simu halafu akamwangalia Margreth kwa tabasamu pana sana kisha akasema
“margreth kila kitu tayari tunaweza kwenda sasa ofisini kwa Andrew”
“You are so fast Patrick”
“Kwa miadi kama hii ya kukutana na Happy kila kitu lazima kiende haraka” Patrick akasema huku akitabasamu
Walitoka hapo Sean snacks na kuelekea moja kwa moja ofisini kwa Andrew.
Iliwachukua kama dakika arobaini hivi kuwasili zilipo ofisi za Andrew.Haraka haraka wakafululiza hadi ofisini.
“Wow Comrade “Akasema Andrew mara tu Patrick alipoingia ofisini kwake.Wakakumbatiana kwa furaha.
“Andrew kutana na Margreth kibaho mdogo wake Happy .Margreth kutana na Andrew,rafiki yangu mkubwa na wa pekee kabisa”
llikuwa ni mara ya kwanza kwa Andrew kumtia machoni Margreth.Macho yake yalijikuta yameganda yakiustaajabia uzuri wa kimwana huyu.
“Mhhhhhh !! mtoto mrembo kama malaika.Ama kweli familia hii imebarikiwa kwa kuwa na watoto warembo .Hapana I have to do something.Hii ni nafasi yangu na mimi” Andrew akawaza.
“Hello Margreth nashukuru sana kukufahamu.Karibu sana”Andrew akasema huku akitoa rabasamu pana sana .
“ Hata mimi nimefurahi sana kukufahamu Andrew....




ITAENDELEA.......


TUPATIE NYOTA 5 KWENYE APP YETU KULE PLAY STORE NA KU COMMENT ILI TUPATE SUPPORT YAKO.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: BINAMU 🔞 SEHEMU YA 11

KIJIJINI KWA BIBI SEHEMU YA 1-5

CHOMBEZO: MASSAGE ROOM🔞 SEHEMU YA 21