UKWELI WENYE KUUMA (PAINFUL TRUTH) SEHEMU YA 70



Simulizi: UKWELI WENYE KUUMA (PAINFUL TRUTH)

Muandishi: NYEMO CHILONGANI

SEHEMU YA 70

Mikakati kabambe ikaandaliwa, vijana nane wakatafutwa, vijana ambao hawakuwa na hata na chembe yoyote ya woga, vijana ambao walikuwa na uzoefu mkubwa wa kutumia bunduki wakati wowote na sehemu yoyote bila kuogopa kitu chochote kile.
Vijana nane tayari walikuwa wamekamilika na kitu ambacho kilifanyika ni kuanza kusafiri kuelekea Tanzania. Kwa kuwa walitumia usafiri wa ndege ya kukodi ambayo ilikuwa ikimilikiwa na Bwana Dawson wala hawakutumia muda mrefu angani wakawa wamekwishafika Tanzania.
Walichokifanya mahali hapo ni kuchukua vyumba katika hoteli ya The Cape na kisha kupumzika. Usiku hawakulala, kitu ambacho walikuwa wakikifanya ni kukusanyika katika chumba kimoja na kuanza kupanga mipango juu ya namna ya kumchukua Andy na kuanza kurudi nae nchini Marekani.
Nchi ya Tanzania wala haikuwaogopesha hata kidogo kwani kwao waliuona ulinzi wa nchi hiyo kuwa ndogo sana na hivyo kuwapa nafasi kubwa sana ya kumchukua Andy salama salimini. Kikao chao cha siri kilichukua dakika thelathini, kila mmoja akaelekea chumbani mwake huku wakimuacha Powell ndani ya chumba kile.
Hawakutaka kuchelewa, siku iliyofuata wakakodi gari moja kwa moja kuanza kuelekea katika sehemu ambayo waliiona kufaa kwa kufanya tukio moja muhimu ambalo walitakiwa kulifanya kwa wakati huo huku wakiwa na bunduki zao zilizokuwa zimejaa risasi.
“Na vipi kuhusu Michael?” Shawn aliuliza
“Amekwishafika jana usiku kwa kutumia boti ile ile ya bosi iendayo kasi. Kinachosubiriwa ni sisi tu” Powell alijibu.
“Na umekwishamwambia wapi pa kuonana?”
“Ndio. Kuna ufukwe unaitwa Coco ambapo hapo ndipo tutakapokutania na kuanza safari yetu. Natumaini hii itakuwa kazi nyepesi sana” Powell alisema huku wakiwa wanaingia eneo la Mnazi Mmoja ikiwa imetimia saa moja na nusu asubuhi.
****
Watanzani walikuwa wakizidi kumiminika ndani ya mahakama kuu ya Tanzania kwa ajili ya kusikiliza hukumu ya kesi hiyo ya mauaji ambayo inamkabili Andy ambayo ilikuwa imevuma kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwili.
Kila mtu alikuwa akitamani hakimu amhukumu kifo Andy kwa kile ambacho alikuwa amekifanya kwa kumuua Spika wa Bunge la Tanzania, Bi Annastazia Kapama. Kadri muda ulivyozidi kwenda mbele na ndivyo ambavyo watu walizidi kuongezeka mahakamani hapo kiasi ambacho watu wengine wakazuiliwa na kutakiwa kusimama nje ya mahakama hiyo.
Kama kawaida, waandishi wa habari walikuwa wakiendelea na kazi yao ya kupiga picha na kuandika mambo mbalimbali ambayo yalikuwa yakiendelea mahali hapo. Ingawa karandinga ilitakiwa kuingia hapo saa mbili kamili asubuhi hiyo lakini watu waliiona karandinga hiyo ikichelewa kufika mahali hapo.

Kama kawaida, waandishi wa habari walikuwa wakiendelea na kazi yao ya kupiga picha na kuandika mambo mbalimbali ambayo yalikuwa yakiendelea mahali hapo. Ingawa karandinga ilitakiwa kuingia hapo saa mbili kamili asubuhi hiyo lakini watu waliiona karandinga hiyo ikichelewa kufika mahali hapo.

“Ni lazima auhukumiwe kifo mjinga yule. Hawezi kutuwekea vidonda mioyoni mwetu” Mwanaume mmoja alisema huku akionekana dhahiri kuwa na hasira.
Muda ulizidi kwenda mbele, saa moja na nusu ikafika, hakimu akawa amekwishafika nje ya mahakama ile lakini bado karandinga halikuwa limeingia mahali hapo. Watu wakaendelea kusubiri zaidi na zaidi, saa mbili kamili ikaingia lakini hali bado ilikuwa vile vile, karandinga halikuwa limeingia mahali hapo jambo ambalo likaonekana kumtia wasiwasi kila mtu.
****
Pikipiki mbili zilikuwa mbele, nyuma ya pikipiki zile kulikuwa na gari aina ya defender ambalo lilikuwa limewapakiza maaskari saba ambao walikuwa na bunduki. Nyuma ya defender ile kulikuwa na karandinga ambalo lilikuwa limewabeba watu ambao walitakiwa kufika mahakamani siku hiyo huku Andy akiwa mmoja wapo.
Ving’ora vilikuwa vikiendelea kusikika hali ambayo iliwataka watu kuyapaki pembeni magari yao kwa ajili ya kuyapisha magari yale ambayo yalikuwa yakielekea Mahakama kuu. Nyuma ya karandinga lile kulikuwa na defender moja ambalo nalo lilikuwa limewabeba maaskari saba waliokuwa na bunduki mikononi mwao.
Walipofika maeneo ya Mnazi Mmoja, kila mmoja akapigwa na mshangao mara baada ya kuona magari mawili ambayo yalikuwa yamepata ajali. Kila polisi alikuwa akishangaa, mazingira ya magari yale kupata ajali yalikuwa yakishangaza na hata kuchekesha, mazingira ambayo kwa mtu ambaye alikuwa na leseni basi hakutahili kupata ajali kama ile.
Magari yote yalikuwa yamesimama huku foleni ikiwa katika eneo hilo. Ving’ora vilisikika zaidi na zaidi lakini hakukuwa na dereva yeyote ambaye alikuwa na uwezo wa kusogeza gari lake kutokana na msongaano wa magari ambao ulikuwa mahali pale.
“Tunazidi kuchelewa kufika mahakamani. Tufanye nini?” Polisi mmoja aliwauliza wenzake.
“Hakuna jinsi. Tushukeni na tujaribu kuyasogeza magari haya upande mwingine na kisha tuende upande mwing ine, natumaini tutaweza kupita” Polisi mmoja alijibu.
Hata kabla hawajafanya kitu chochote kile, polisi mmoja akaanguka chini, damu zilikuwa zikimtoka kifuani huku akitupa miguu na mikono yake kila upande. Kila polisi ambaye alikuwa akimwangalia polisi yule alikuwa akipigwa na mshangao, hali ambayo ilikuwa imetokea haikuonekana kueleweka mbele ya macho yao.
Wala hazikupita hata sekunde kumi, mapolisi wawili wakaanguka chini, damu zilikuwa zikiwatoka vifuani. Hapo ndipo walipopata picha kwamba kulikuwa na kitu ambacho kilikuwa kinaendelea mahali hapo. Walichokifanya mapolisi wale ni kupiga risasi hewani, watu wakaanza kukimbia ovyo.
Mapolisi ambao walikuwa katika defender ya nyuma wakaanza kuja kule mbele huku wakiwa wameziweka sawa bunduki zao. Tayari waliona kwamba kulikuwa na kitu ambacho kilikuwa kinaendelea, wakaanza kulipa ulinzi zaidi karandinga lile.
Kila walipokuwa wakiangalia wala hawakuweza kumuona mtu yeyote ambaye alikuwa na bunduki au hata kuisikia milio ya bunduki za maadui zao. Mapolisi bado walikuwa wakianguka chini mmoja baada ya mwingine, risasi zilikuwa zikiendelea kuingia miilini mwao.


ITAENDELEA.......



TUPATIE NYOTA 5 KWENYE APP YETU KULE PLAY STORE NA KU COMMENT ILI TUPATE SUPPORT YAKO.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: BINAMU 🔞 SEHEMU YA 11

KIJIJINI KWA BIBI SEHEMU YA 1-5

CHOMBEZO: MASSAGE ROOM🔞 SEHEMU YA 21