Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2022

MIMBA YA JINI SEHEMU YA 3

Picha
MIMBA YA JINI 03 ILIPOISHIA: "Basi bosi kapumzishe akili utajua pete umeiweka wapi." Mustafa alirudi ofisini kwake na kukaa kitini, alijitazama vidole vyake asiamini kama kweli hakuja na pete. Akiwa bado anavishangaa vidole vyake simu yake iliita, alipoangalia alikuta ni Shehna. Aliipokea: SASA ENDELEA..." Haloo." "Haloo Mustafa samahani, niliwahi kutoka kwa vile kuna sehemu nilitakiwa kuwahi." "Umepitia wapi?" "Jamani Mustafa kuna njia ngapi ya kuingia na kutokea ofisini kwako?" "Moja." "Basi ndiyo niliyopitia." "Mbona sekretari wangu hajakuona?" "Nimemkuta yupo bize ila sikutaka kumsumbua kwa vile mlango wako ulikuwa wazi." "Huyo hajakuona, na mlinzi?" "Sikumkuta inawezekana alikuwa msalani." "Mmh!" "Mustafa unaguna nini?" "Aah! Basi yaani bado ujio wako umekuwa kitendawili, pete yangu umechukua?" "Mustafaa! Niichukue ili iweje tuna uhusiano...

ADUI WA MAISHA SEHEMU YA 3

Picha
SIMULIZI: ADUI WA MAISHA MTUNZI: LISSA WA MARIAM SEHEMU YA TATU Lameck alisema na kuamua kumpeleka Isabella chumbani kwake, alimuwashia laptop na kuweka movie, yeye akatoka nje hazikupita dakika nyingi alirudi na kukaa karibu yake, waliongea wakataniana, wakachekeshana, wakacheza kama watoto mwisho Lameck alipeleka midomo yake kwenye midomo ya Isabella, wakabadirishana mate, Lameck hakuishia hapo alipeleka mikono yake kwenye chuchu za Isabella "Mmh Lameck please don't do anything" Isabella aliongea kwa sauti ya chini na kumtoa Lameck mikono "Baby sifanyi kitu kibaya tunacheza tu" Lameck alijitahidi kubembeleza, Alitumia kila mbinu mwisho wa siku akajikuta anamshinda Isabella na kilichotokea ni kelele kutoka kwa binti huyo, alilia kupita maelezo tayari alikuwa ameshapoteza usichana wake, hasira zilimpanda lakini hakuwa na chakufanya, zoezi halikuwa la muda mrefu Lameck alimaliza kazi yake, "Pole baby sikujua kabisa Kama nitakuumiza" "Sitaki kuongea...

KURUDI KWA MOZA SEHEMU YA 5

Picha
KURUDI KWA MOZA SEHEMU YA 5 MTUNZI: ATUGANILE MWAKALILE Hapo akazimia, na lilipita lisaa limoja akazinduka akiwa amechoka sana, akajaribu kuinuka akaweza, kisha akatoka na kufunga mlango halafu funguo akazirudishia pale pale juu. Akaelekea sebleni sasa, Mara akakutana na mama mwenye nyumba nae anaingia sebleni kutoka nje akiwa na hasira sana. Alikuwa anahema juu juu, akamsogelea Moza na kumuuliza kwa ukali “Umefanya nini?” “Sijafanya chochote mama” Rose alimuacha Moza pale sebleni na kuelekea mitaa ya chumbani ambapo moja kwa moja alielekea kwenye kile chumba, Moza alienda jikoni huku uoga ukiwa umemshika na kuomba kuwa huyu mama asijue kama aliingia mule chumbani. Ingawa moza alikuwa kamaliza kupika ila alikaa tu jikoni akiwaza, muda kidogo Rose alirudi sebleni na kumuita Moza kwa ukali, kitendo ambacho kilimuogopesha Moza na kuhisi kuwa pengine Rose amegundua. Alienda sebleni kwa uoga kiasi, kisha huyu mama akamuuliza, “Baba aliamka toka ameenda kulala?” “Hapana mama, toka muda ule s...

VITA YA WACHAWI SEHEMU YA 7

Picha
VITA YA WACHAWI 07 MTUNZI ALLY MBETU “Mchumba niliyetaka kumuoa kachukuliwa na mamba katika mazingira ya kutatanisha,” alimweleza mengine japo mwanzo hakumwambia. “Mungu wangu pole sana,” Atuganile alijifanya kushtuka. “Si bure lazima kuna mkono wa mtu.” “Lakini mpenzi usisikitike sana mimi mpenzi wako wa damu si nipo?” “Sawa, lakini huoni kama wanaweza kutufikiria vibaya labda tumepanga kumpoteza ili tuendelee kuwa pamoja. Japo tuko pamoja lazima kipindi hicho uhusiano wetu usiwe wa wazi sana kuonana kwetu iwe usiku tu.” “Sawa, lakini sikubali utafutiwe mwanamke mwingine kama amepotea au amekufa nasubiri ndoa yangu.” “Hakuna tatizo, kama hivyo sitakubali kuchaguliwa tena mwanamke,” Ambakisye alimuhakikishia mpenzi wake. “Nimefurahi kusikia hivyo, basi naomba utumie hii dawa ili tujue tatizo nini.” “Mmh! Sawa, lakini lazima nizungumze na baba ili nijue ataniambiaje.” “Amba kwa nini usitumie tu ili tujue kitakuwa nini kuliko kuwapa presha wazazi wako?” “Hapana lazima nimwambie baba kwa ...

KOVU LA MOYO SEHEMU YA 7

Picha
KOVU LA MOYO 07 MTUNZI: DEE LOVEE "Mambo vipi Jonas" ... Robby alimsalimia kisha Poshie na Angelo pia wakafanya hivyo ... "Jonas huyu si unamfahamu?" .... Robby alimuuliza huku akimuoneshea Angelo ... "namjua ndiyo si Angelo huyo" ... "Vizuri kama unamjua. Huyu Mshikaji bwana alikuwa na matatizo yeye pamoja na mpenzi wake, kwa ufupi ni kwamba Mpenzi wake amefukuzwa kwao na amesusiwa yeye. Mimi niliwasaidia ila Bi Mkubwa amegoma na amewatimua, sasa mshikaji hana pa kulala na mimi naondoka naelekea Uganda naenda kusoma, sasa nilikuwa naomba wajishikize katiika geto lako mpaka Mshikaji atakapo pata kazi basi atachukua chumba chake" ... Robby alimwambia Jonas kwa umakini sana lakini cha ajabu alipomaliza kuongea Jonas alicheka sana na kumwambia ... "Hapa mtaani watu wanakusifu sana Robby kuwa una akili lakini kwa ili umechemka mchizi wangu. Unapata tabu kwa matatizo ya kujitakia? Yeye kajitakia majukumu mwenyewe basi muache aangaike mwenyewe, ya...

WAKILI WA MOYO SEHEMU YA 16

Picha
WAKILI WA MOYO SEHEMU: 16 MTUNZI: Ally Mbetu ‘Dr Ambe’ ILIPOISHIA: “Hakuna tatizo.” Hans aligeuza gari na kuelekea Masaki, muda wote Mage alikuwa amejilaza kwenye siti baada ya kuilaza kwa nyuma. Hans alisimamisha gari kwenye maegesho ya Sea Cliff hoteli. SASA ENDELEA... “Bebi tumefika,” alimshtua Mage aliyekuwa amefumba macho. “Kachukua chumba kabisa,” Mage alijibu bila kufumbua macho. “Sawa.” Hans aliteremka na kwenda kulipia chumba kisha alirudi kumweleza Mage. “Tayari.” Aliteremka na kufunga gari lao kisha waliongozana hadi ndani ya chumba walichokikodi. Mage alipofika alijilaza kitandani macho alitazama juu mikono alilalia kwa nyuma. Pembeni ya macho yake michirizi ya machozi iliendelea kuteremka na kulowesha shuka. “Vipi bebi?” Hans alizidi alishtuka. “Hans sijui nikueleze nini uelewe najua jamii itanitenga kwa ajili ya uamuzi wangu wa kuvunja uchumba, wapo watakao niona sina akili lakini anayejua mapenzi ataniunga mkono. Nimekubali kubeba lawama zote za wanadamu lakini niufurahi...

MWANAMKE JINI SEHEMU YA 18

Picha
MWANAMKE JINI SEHEMU YA 18 MTUNZI: FAKI A FAKI ILIPOISHIA “Yule mzee alinyamaza kimya akitafakari kwa sekunde zisizopungua tano kisha akaniuliza. “Huyo msichana ni nani wako?” “Tunafahamiana tu, tulikuwa tumekaa tunazungumza” “Sasa nataka kukueleza kitu kimoja. Mmoja wa wale vijana waliompora huyo msichana ni mwanangu. Jana usiku aliporudi nyumbani hatukulala” “Kwanini?” “Yule kijana alipoingia chumbani mwake tulisikia anapiga kelele. Mimi nikaenda kumuuliza ana matatizo gani, akaniambia kwamba kila anapopitiwa na usingizi anamuona mwanamke anampiga bakora. Nikamuuliza ni mwanamke gani huyo, ndio akanieleza kwamba kuna mwanamke walimpora mkoba wake na ndiye huyo anayemuona anampiga bakora. “Hiyo hali iliendelea hadi asubuhi, kila akifumba macho tu anamuona, anamtandika. Bakora zimeota mgongoni mwake. Huyo mwanamke haonekani, anamuona yeye tu pale anapolala. “Hii asubuhi tukaenda kwa huyo mwenzake, kumbe na yeye hali ni hiyo hiyo. Amepigwa bakora usiku kucha. Bakora zimeota kwenye mgong...

MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN SEHEMU YA 18

Picha
MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN -- 018 Simulizi za series Kusikia jina la Faki, tena katikati ya shughuli nzito kama ile, haikuwa habari nzuri kabisa. Vikongwe walitinduka akili. Walitazamana katika macho ya kujiuliza nini cha kufanya, na bahati mbaya zaidi muda haukuwepo upande wao. Haraka mmoja aliunyanyua mwili wa Malkia na kukimbia nao chumbani. Kitabu na mkasi vilitupiwa kando, ila kwakuwa muda haukutosha kuondosha kila kitu kitakachozua maswali, basi yakaachwa mengineyo. Kikongwe mmoja akaufuata mlango na kuufungua. Macho yake yalikutana ana kwa ana na bwana Faki aliyekuwa anatabasamu, tabasamu la kinafki. Mwanaume huyo alikuwa amevalia suti nyeusi za mtindo poa wa kale. Nywele zake zilikuwa zimelala kana kwamba zimemiminiwa mafuta malaini. Uso wake, ufananao na wa fisi kwa namna zote, ulikuwa umezingirwa na ndevu zilizotindwa vema. Macho yake madogo yenye kona nyembamba yalikuwa yamezingirwa na rangi nyeusi. Kwa kuhitimisha, chini aling’ara kwa viatu vyeusi viangavu. “Unahitaji nini k...

MZIMU UMERUDI TENA EPISODE:29

Picha
MZIMU UMERUDI TENA. EPISODE:29 MTUNZI;HAMIDU MCHAKO ....................TULIPOISHIA.............. Nikiwa nahangaika kumpokonya niliwaona watu wawili wamemshika baba na wamemnyooshea bastola waliniambia tulia na achia hilo begi laa sivyo tunamwaga ubongo........... ..........ENDELEA.......... Niliduwaa kidogo na nikagundua tumetekwa bali hatukupelekwa gest. Nilimtazama kwa hasira yule dereva halafu ch kustaajabisha hakuwa na wasi wasi wowote. Nilianza kufikiria baba na begi la pesa kipi nipoteze? Niligundua baba anadhamani kuliko pesa hivyo sikua na jinsi niliamua niwakabidhi lile begi la fedha ila kabla sikuwakabidhi niliwauliza. ➡Jeee tukisha wakabidhi hili begi mtatuacha huru? Walijibu ndio tutawaachia huru. Moyo wangu ulifarijika kuwa watatuacha huru na wakituacha huru tutarudi kuja kupambana ili waturudishie pesa zetu. Niliwakabidhi lile begi na baada ya kutusachi na kugundua kuwa hatuna silaha yeyote walituachia. Lile begi Alipewa mtu mmoja na alionekana ndio kiongozi wa kikundi k...