KURUDI KWA MOZA SEHEMU YA 5
KURUDI KWA MOZA
SEHEMU YA 5
MTUNZI: ATUGANILE MWAKALILE
Hapo akazimia, na lilipita lisaa limoja akazinduka akiwa amechoka sana, akajaribu kuinuka akaweza, kisha akatoka na kufunga mlango halafu funguo akazirudishia pale pale juu. Akaelekea sebleni sasa, Mara akakutana na mama mwenye nyumba nae anaingia sebleni kutoka nje akiwa na hasira sana. Alikuwa anahema juu juu, akamsogelea Moza na kumuuliza kwa ukali
“Umefanya nini?”
“Sijafanya chochote mama”
Rose alimuacha Moza pale sebleni na kuelekea mitaa ya chumbani ambapo moja kwa moja alielekea kwenye kile chumba, Moza alienda jikoni huku uoga ukiwa umemshika na kuomba kuwa huyu mama asijue kama aliingia mule chumbani. Ingawa moza alikuwa kamaliza kupika ila alikaa tu jikoni akiwaza, muda kidogo Rose alirudi sebleni na kumuita Moza kwa ukali, kitendo ambacho kilimuogopesha Moza na kuhisi kuwa pengine Rose amegundua. Alienda sebleni kwa uoga kiasi, kisha huyu mama akamuuliza,
“Baba aliamka toka ameenda kulala?”
“Hapana mama, toka muda ule sijamuona tena sebleni?”
“Sikia Moza, naomba vitu vya nyumba hii uviache kama vilivyo”
“Ila sijafanya kitu mama”
“Nilikuwa mbali sana, ila kuna kitu kimefanyika ndani nimepata taarifa ndiomana nikaja haraka sana. Ila kwavile umesema hujafanya kitu, basi. Hata hivyo hicho kitu ambacho nilikuwa nakihisi kuwa umekifanya basi muda huu ningekukuta na hali mbaya sana. Tafadhali Moza, vitu vya nyumba hii viache kama vilivyo. Unaweza ukanishangaa kuwa mbona narudia rudia msemo wangu, nina maana kabisa, viache kama vilivyo”
“Sawa mama nimekuelewa”
“Na sitoki tena saivi,ngoja nikapumzike tu. Nipikie ugali na samaki, nitakula nikiamka”
Moza alienda jikoni kuandaa huo ugali huku akiwaza kuwa amepona ila aliwaza ameponapona vipi bila kubambwa ingawa alizimia kwa karibu lisaa lizima, pia akawaza kuwa huyu mama kapata vipi taarifa huko alipokuwa kwamba ule mlango ulishikwa? Hapo kidogo akapatwa na uoga, akawa tu anajisemea mwenyewe
“Mimi Moza mimi jamani nitulie tu, kwetu nakupenda pia. Nitakuwa sirudi mmmh”
Alipomaliza alienda chumbani mara moja.
ITAENDELEA........
TUPATIE NYOTA 5 KWENYE APP YETU KULE PLAY STORE NA KU COMMENT ILI TUPATE SUPPORT YAKO.
Maoni
Chapisha Maoni