MWANAMKE JINI SEHEMU YA 18



MWANAMKE JINI

SEHEMU YA 18

MTUNZI: FAKI A FAKI

ILIPOISHIA
“Yule mzee alinyamaza kimya akitafakari kwa sekunde zisizopungua tano kisha akaniuliza.
“Huyo msichana ni nani wako?”
“Tunafahamiana tu, tulikuwa tumekaa tunazungumza”
“Sasa nataka kukueleza kitu kimoja. Mmoja wa wale vijana waliompora huyo msichana ni mwanangu. Jana usiku aliporudi nyumbani hatukulala”
“Kwanini?”
“Yule kijana alipoingia chumbani mwake tulisikia anapiga kelele. Mimi nikaenda kumuuliza ana matatizo gani, akaniambia kwamba kila anapopitiwa na usingizi anamuona mwanamke anampiga bakora. Nikamuuliza ni mwanamke gani huyo, ndio akanieleza kwamba kuna mwanamke walimpora mkoba wake na ndiye huyo anayemuona anampiga bakora.
“Hiyo hali iliendelea hadi asubuhi, kila akifumba macho tu anamuona, anamtandika. Bakora zimeota mgongoni mwake. Huyo mwanamke haonekani, anamuona yeye tu pale anapolala.
“Hii asubuhi tukaenda kwa huyo mwenzake, kumbe na yeye hali ni hiyo hiyo. Amepigwa bakora usiku kucha. Bakora zimeota kwenye mgongo wake. Kwa kweli nimewagombesha sana wale vijana kwa kututia aibu sisi wazazi wao kwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu wakiwa bado wadogo, kuibia watu, kupiga watu na kuvuta bangi. Imebidi niwaulize ni mwanamke gani huyo waliyempora mkoba wake ndipo mwanangu aliponielekeza kwako. Kumbe alikuwa anakufahamu.
“Sasa mwanangu nimekuja, nakuomba unioneshe yule mwanamke nimlipe ule mkoba wake na nimuombe radhi ili wale vijana waondokewe na ile hali”
Yale maneno aliyonieleza yule mzee yalinishangaza na kunishitua. Wakati yule mzee ananieleza mimi nilikuwa natokwa na jasho.
“Kwani mpaka hii asubuhi wanaendelea kuchapwa bakora?’ nikamuuliza.
“Labda wakae bila kusinzia au kulala. Wanapolala kidogo tu tayari wanapiga kelele wanasema wanachapwa. Ni mpaka hii asubuhi hawajalala tangu jana wako macho tu. Wameshadhoofika. Kama hii hali itaendelea watakufa”
“Mzee wangu nikwambie ukweli, yule mwanamke tulikutana pale pale. Sijui anapoishi na sidhani kama nitamuona tena”

SASA ENDELEA
Mzee akashituka na kujishika kichwa.
“Mimi nilidhani unajuana na huyo mwanamke. Basi wale vijana hawatakuwa na maisha tena” Mzee akasema kisha akaniuliza.
“Unasema kweli, hujuani naye kabisa?’
“Sijuani naye mzee wangu, siwezi kukudanganya. Tulikutana pale pale, kila mmoja alikuja kivyake na aliondoka kivyake’
Mzee aliduwaa kwa sekunde zisizopungua kumi, alipozinduka aliniuliza.
“Hivi mwanangu utanisaidiaje na balaa hili?”
“Mzee wangu sina namna yoyote ya kukusaidia”
“Tuseme yule mwanamke alikwenda kwa mganga kuwaroga wale vijana?”
“Kwa waswahili hilo jambo linawezekana lakini siwezi kujua”
“Sasa nifanyeje?”
Sikumjibu yule mzee. Alionesha wazi alikuwa amechanganykiwa. Alipoona nipo kimya, aligeuka bila kuniaga na kushuka kwenye baraza ya nyumba yangu. Nikamsikia akisema peke yake.
“Kama hawatakoma, hawatakoma tena!”
Alipofika chini ya baraza ndipo alipokumbuka kuniaga.
“Haya kwaheri mwanangu” akaniambia.
Nilimuangalia yule mzee hadi alipokata kona mtaa wa pili, lakini mawazo yangu yalikuwa kwa Zena. Kitendo kile cha kuwatandika wale vijana bakora kilionesha kuwa mwanamke yule wa kijini alikuwa wa hatari.
Nilikumbuka wakati wale vijana wamempora mkoba wake alionekana mtulivu ingawa alionesha kuwa na hasira. Aliniambia “Waache tu” kumbe alikuwa na lake alilokuwa amelipanga.
Japokuwa niliwahurumia hao vijana lakini sikujua ningempata wapi huyo Zena ili nimwambie awasamehe hao vijana. Na hata kama ningekutana naye na kumwambia hivyo sikudhani kama angenisikia.
Nilirudi ndani na kuendelea kujiwazia. Nilihisi kwamba hata mimi maisha yangu yangeweza kuwa katika hatari kama nitakataa kumuoa Zena na kwa kweli hata hapo nitakapokutana naye nitashindwa kumueleza ukweli kwamba sikubaliani na matakwa yake ya kumuoa.
Kwa vyovyote vile yule mwanamke anaweza kunidhuru!
Nilipowaza hivyo nilitoka tena. Nikafunga mlango wangu na kuondoka na pikipiki yangu, nikaenda nyumbani kwa mama.
Kitendo cha kurudi tena kwa mama kilimshitua, akaniuliza.
“Kulikoni?”
“Nimerudi tena” nikamwambia.
“Ndio mana nimekuuliza kulikoni?”
Nikamueleza mama kile kisa cha yule jini kuwatandika bakora wale vijana waliomuibia mkoba wake.
“Baba wa mmoja wa wale vijana ameniambia hao vijana hivi sasa wako taabani wanamtafuta yule msichana wamuombe msamaha” nikamwambia.
Mama naye alishituka.
“Yaani wanapolala ndio wanamuona huyo msichana anawatandika bakora?”
“Ndio mama, na inakuwa usiku kucha na mchana kutwa. Miili ya wale vijana imeota makora migongoni”
“Huyo jini ni mbaya sana”
“Sasa nimefikiri hata mimi anaweza kuja kuniletea madhara kama nitakataa kumuoa”
“Ni kweli, sasa nikupeleke kwa mganga”
“Wapi?”
“Kule Mnyanjani, ni hodari sana kwa majini”
“Ndio maana nimekuja ili tushauriane kwenda kwa huyo mganga, vinginevyo naweza kupata balaa”
“Sasa nikupeleke lini?”
“Leo, twende leo”
“Saa ngapi?’
“Maliza kazi zako nitakufuata saa tisa twende”
“Sawa. Basi njoo hapo saa tisa twende”
Tulipokubaliana na mama nikaondoka. Wakati nafika nyumbani kwangu nikakutana na yule mzee akiondoka.
“Nimegonga mlango, nimeona kimya. Nilikuwa naenda zangu” akaniambia.
“Nilitoka kidogo”
“Nimekuja kukujulisha kuwa yule mwanangu ameshafariki dunia”
Nikashituka.
“Eh ameshafariki!”
“Amefariki kama nusu saa hivi iliyopita akiwa kwa mganga. Tulikuwa tumempeleka kwa mganga baada ya mateso kumzidia”
“Poleni sana jamani. Yule mwenzake naye anaendeleaje?’
“Sijapata habari zake. Nimekuja kukwambia hivyo, kwaheri mwanangu”
Mzee huyo akaondoka. Nilipata hofu sana. Sikuweza hata kuingia ndani. Niliona kama vile nitakutana na jini huyo, nikageuza pikipiki na kurudi kwa mama.
Nilipofika nilimuhadithia lile tukio la kufa kwa mmoja wa wale vijana.
“Nimekuja nikusubri hapa hapa, sikuingia hata nyumbani kwangu” nikamwambia.
Chakula cha mchana nilikula pale pale kwa mama. Baada ya kula ndipo tulipoondoka. Nilimpakia mama kwenye pikipiki tukaelekea huko Mnyanjani.
Wakati huo eneo hilo la Mnyanjani lilikuwa kama kitongoji cha mji huo. Likiwa karibu na ufukwe wa Bahari ya Hindi, lilikuwa moja ya maeneo ya kiasili ya mji wa Tanga yenye historia iliyosheheni utamaduni wa jiji hilo.
Eneo hilo hivi sasa limebadilika na kuwa na nyumba za kisasa na kuwa sehemu ya jiji hilo.
Ili ufike Mnyanjani unapita vitongoji kadhaa pamoja na viunga vya minazi. Ni mwendo wa karibu kilometa kumi.
Mama alinionesha nyumba ya mganga huyo iliyokuwa imejengwa kwa miti na udongo na kuezekwa makuti ya minazi.
Tukasimama na kubisha mlango.
“Karibuni” tukasikia sauti ya kiume ikitukaribisha.
Tukaingia ndani. Ukumbi ulikuwa giza. Kulikuwa na mwanga hafifu uliotokea kwenye mlango wa nje na wa uani.
Mganga mwenyewe alikuwa amekaa kwenye jamvi lililokuwa limetandikwa pale ukumbini. Alikuwa akikatakata mizizi ya dawa.
“Karibuni” akatuambia tena huku akitutazama.
“Tumeshakaribia” mama akamwambia na kisha kumuuliza hali.
Mimi nikamuamkia. “Shikamoo”
“Marahaba. Karibuni mkake kwenye jamvi”
Tukakaa kwenye jamvi.
“Tumekuja tuna shida” Mama akaanza kumwambia mzee huyo aliyekuwa amevaa kikoi cha rangi nyeupe.
“Shida gani?”
MAMBO YAMEFIKA KWA WAGANGA. JE MGANGA HUYO ATAWEZA KUPAMBANA NA MWANAMKE HUYO WA KIJINI AMBAYE AMESHAONESHA SI WA KUCHEZEA?
MWANAMKE JINI: SEHEMU YA 18
MTUNZI: FAKI A FAKI

ILIPOISHIA
“Yule mzee alinyamaza kimya akitafakari kwa sekunde zisizopungua tano kisha akaniuliza.
“Huyo msichana ni nani wako?”
“Tunafahamiana tu, tulikuwa tumekaa tunazungumza”
“Sasa nataka kukueleza kitu kimoja. Mmoja wa wale vijana waliompora huyo msichana ni mwanangu. Jana usiku aliporudi nyumbani hatukulala”
“Kwanini?”
“Yule kijana alipoingia chumbani mwake tulisikia anapiga kelele. Mimi nikaenda kumuuliza ana matatizo gani, akaniambia kwamba kila anapopitiwa na usingizi anamuona mwanamke anampiga bakora. Nikamuuliza ni mwanamke gani huyo, ndio akanieleza kwamba kuna mwanamke walimpora mkoba wake na ndiye huyo anayemuona anampiga bakora.
“Hiyo hali iliendelea hadi asubuhi, kila akifumba macho tu anamuona, anamtandika. Bakora zimeota mgongoni mwake. Huyo mwanamke haonekani, anamuona yeye tu pale anapolala.
“Hii asubuhi tukaenda kwa huyo mwenzake, kumbe na yeye hali ni hiyo hiyo. Amepigwa bakora usiku kucha. Bakora zimeota kwenye mgongo wake. Kwa kweli nimewagombesha sana wale vijana kwa kututia aibu sisi wazazi wao kwa kujihusisha na vitendo vya kihalifu wakiwa bado wadogo, kuibia watu, kupiga watu na kuvuta bangi. Imebidi niwaulize ni mwanamke gani huyo waliyempora mkoba wake ndipo mwanangu aliponielekeza kwako. Kumbe alikuwa anakufahamu.
“Sasa mwanangu nimekuja, nakuomba unioneshe yule mwanamke nimlipe ule mkoba wake na nimuombe radhi ili wale vijana waondokewe na ile hali”
Yale maneno aliyonieleza yule mzee yalinishangaza na kunishitua. Wakati yule mzee ananieleza mimi nilikuwa natokwa na jasho.
“Kwani mpaka hii asubuhi wanaendelea kuchapwa bakora?’ nikamuuliza.
“Labda wakae bila kusinzia au kulala. Wanapolala kidogo tu tayari wanapiga kelele wanasema wanachapwa. Ni mpaka hii asubuhi hawajalala tangu jana wako macho tu. Wameshadhoofika. Kama hii hali itaendelea watakufa”
“Mzee wangu nikwambie ukweli, yule mwanamke tulikutana pale pale. Sijui anapoishi na sidhani kama nitamuona tena”

SASA ENDELEA
Mzee akashituka na kujishika kichwa.
“Mimi nilidhani unajuana na huyo mwanamke. Basi wale vijana hawatakuwa na maisha tena” Mzee akasema kisha akaniuliza.
“Unasema kweli, hujuani naye kabisa?’
“Sijuani naye mzee wangu, siwezi kukudanganya. Tulikutana pale pale, kila mmoja alikuja kivyake na aliondoka kivyake’
Mzee aliduwaa kwa sekunde zisizopungua kumi, alipozinduka aliniuliza.
“Hivi mwanangu utanisaidiaje na balaa hili?”
“Mzee wangu sina namna yoyote ya kukusaidia”
“Tuseme yule mwanamke alikwenda kwa mganga kuwaroga wale vijana?”
“Kwa waswahili hilo jambo linawezekana lakini siwezi kujua”
“Sasa nifanyeje?”
Sikumjibu yule mzee. Alionesha wazi alikuwa amechanganykiwa. Alipoona nipo kimya, aligeuka bila kuniaga na kushuka kwenye baraza ya nyumba yangu. Nikamsikia akisema peke yake.
“Kama hawatakoma, hawatakoma tena!”
Alipofika chini ya baraza ndipo alipokumbuka kuniaga.
“Haya kwaheri mwanangu” akaniambia.
Nilimuangalia yule mzee hadi alipokata kona mtaa wa pili, lakini mawazo yangu yalikuwa kwa Zena. Kitendo kile cha kuwatandika wale vijana bakora kilionesha kuwa mwanamke yule wa kijini alikuwa wa hatari.
Nilikumbuka wakati wale vijana wamempora mkoba wake alionekana mtulivu ingawa alionesha kuwa na hasira. Aliniambia “Waache tu” kumbe alikuwa na lake alilokuwa amelipanga.
Japokuwa niliwahurumia hao vijana lakini sikujua ningempata wapi huyo Zena ili nimwambie awasamehe hao vijana. Na hata kama ningekutana naye na kumwambia hivyo sikudhani kama angenisikia.
Nilirudi ndani na kuendelea kujiwazia. Nilihisi kwamba hata mimi maisha yangu yangeweza kuwa katika hatari kama nitakataa kumuoa Zena na kwa kweli hata hapo nitakapokutana naye nitashindwa kumueleza ukweli kwamba sikubaliani na matakwa yake ya kumuoa.
Kwa vyovyote vile yule mwanamke anaweza kunidhuru!
Nilipowaza hivyo nilitoka tena. Nikafunga mlango wangu na kuondoka na pikipiki yangu, nikaenda nyumbani kwa mama.
Kitendo cha kurudi tena kwa mama kilimshitua, akaniuliza.
“Kulikoni?”
“Nimerudi tena” nikamwambia.
“Ndio mana nimekuuliza kulikoni?”
Nikamueleza mama kile kisa cha yule jini kuwatandika bakora wale vijana waliomuibia mkoba wake.
“Baba wa mmoja wa wale vijana ameniambia hao vijana hivi sasa wako taabani wanamtafuta yule msichana wamuombe msamaha” nikamwambia.
Mama naye alishituka.
“Yaani wanapolala ndio wanamuona huyo msichana anawatandika bakora?”
“Ndio mama, na inakuwa usiku kucha na mchana kutwa. Miili ya wale vijana imeota makora migongoni”
“Huyo jini ni mbaya sana”
“Sasa nimefikiri hata mimi anaweza kuja kuniletea madhara kama nitakataa kumuoa”
“Ni kweli, sasa nikupeleke kwa mganga”
“Wapi?”
“Kule Mnyanjani, ni hodari sana kwa majini”
“Ndio maana nimekuja ili tushauriane kwenda kwa huyo mganga, vinginevyo naweza kupata balaa”
“Sasa nikupeleke lini?”
“Leo, twende leo”
“Saa ngapi?’
“Maliza kazi zako nitakufuata saa tisa twende”
“Sawa. Basi njoo hapo saa tisa twende”
Tulipokubaliana na mama nikaondoka. Wakati nafika nyumbani kwangu nikakutana na yule mzee akiondoka.
“Nimegonga mlango, nimeona kimya. Nilikuwa naenda zangu” akaniambia.
“Nilitoka kidogo”
“Nimekuja kukujulisha kuwa yule mwanangu ameshafariki dunia”
Nikashituka.
“Eh ameshafariki!”
“Amefariki kama nusu saa hivi iliyopita akiwa kwa mganga. Tulikuwa tumempeleka kwa mganga baada ya mateso kumzidia”
“Poleni sana jamani. Yule mwenzake naye anaendeleaje?’
“Sijapata habari zake. Nimekuja kukwambia hivyo, kwaheri mwanangu”
Mzee huyo akaondoka. Nilipata hofu sana. Sikuweza hata kuingia ndani. Niliona kama vile nitakutana na jini huyo, nikageuza pikipiki na kurudi kwa mama.
Nilipofika nilimuhadithia lile tukio la kufa kwa mmoja wa wale vijana.
“Nimekuja nikusubri hapa hapa, sikuingia hata nyumbani kwangu” nikamwambia.
Chakula cha mchana nilikula pale pale kwa mama. Baada ya kula ndipo tulipoondoka. Nilimpakia mama kwenye pikipiki tukaelekea huko Mnyanjani.
Wakati huo eneo hilo la Mnyanjani lilikuwa kama kitongoji cha mji huo. Likiwa karibu na ufukwe wa Bahari ya Hindi, lilikuwa moja ya maeneo ya kiasili ya mji wa Tanga yenye historia iliyosheheni utamaduni wa jiji hilo.
Eneo hilo hivi sasa limebadilika na kuwa na nyumba za kisasa na kuwa sehemu ya jiji hilo.
Ili ufike Mnyanjani unapita vitongoji kadhaa pamoja na viunga vya minazi. Ni mwendo wa karibu kilometa kumi.
Mama alinionesha nyumba ya mganga huyo iliyokuwa imejengwa kwa miti na udongo na kuezekwa makuti ya minazi.
Tukasimama na kubisha mlango.
“Karibuni” tukasikia sauti ya kiume ikitukaribisha.
Tukaingia ndani. Ukumbi ulikuwa giza. Kulikuwa na mwanga hafifu uliotokea kwenye mlango wa nje na wa uani.
Mganga mwenyewe alikuwa amekaa kwenye jamvi lililokuwa limetandikwa pale ukumbini. Alikuwa akikatakata mizizi ya dawa.
“Karibuni” akatuambia tena huku akitutazama.
“Tumeshakaribia” mama akamwambia na kisha kumuuliza hali.
Mimi nikamuamkia. “Shikamoo”
“Marahaba. Karibuni mkake kwenye jamvi”
Tukakaa kwenye jamvi.
“Tumekuja tuna shida” Mama akaanza kumwambia mzee huyo aliyekuwa amevaa kikoi cha rangi nyeupe.
“Shida gani?”
MAMBO YAMEFIKA KWA WAGANGA. JE MGANGA HUYO ATAWEZA KUPAMBANA NA MWANAMKE HUYO WA KIJINI AMBAYE AMESHAONESHA SI WA KUCHEZEA?


ITAENDELEA.......


TUPATIE NYOTA 5 KWENYE APP YETU KULE PLAY STORE NA KU COMMENT ILI TUPATE SUPPORT YAKO.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: BINAMU 🔞 SEHEMU YA 11

KIJIJINI KWA BIBI SEHEMU YA 1-5

CHOMBEZO: MASSAGE ROOM🔞 SEHEMU YA 21