Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2022

ANGA LA WASHENZI SEHEMU YA 1

Picha
ANGA LA WASHENZI -- 001 Simulizi_za_series Mvua ilikuwa inanyesha sana. Hali ya hewa ilikuwa baridi ikiambatana na upepo wa wastani. Watu wengi hawakwenda kazini, na hata wanafunzi pia wakitega shule kwa kisingizio cha barabara kufurika maji. . . . Pengine watu hawa walikuwa na hoja kutokana na miundombinu dhaifu ya jiji la Dar es Salaam ambayo haiwezi kurandana na mikikimikiki ya mvua. Ila kwa mwanaume Jonathan Mchau, hilo halikuwa na mashiko kamili kwani yeye alikuwa ofisini akiendelea na kazi zake kama ilivyo ada. . . . Ni ndani ya chumba kidogo kinachopatikana maeneo ya mwenge. Kwenye kuta za chumba hicho kulikuwa kumetundikwa picha kadhaa za kuchorwa kwa mikono. Picha hizi zilikuwa zimeundwa kimafumbo lakini pia zikibeba utajiri wa tamaduni za Afrika kwa ujumla. . . . Kama ungelipata nafasi ya kutembelea hapo basi ungepatwa na kamshangao kidogo kutazama picha hizo zilizofumwa na rangi mbalimbali za kuvutia kiasi kwamba ukasahau kuwa eneo hilo limepakana na barabara yenye makelele ...

JOANA ANAONA KITU USIKU SEHEMU YA 1

Picha
* JOANA ANAONA KITU USIKU!* 01 *Simulizi za series inc.* Jua linapozama, Joana hukosa raha. Si kwasababu anaishi Brussels, Ubelgiji, kipindi hiki cha baridi, la hasha! Bali kwasababu usiku huwa mzito sana kwake. Punde giza linapoingia, anapoteza amani na mwili wake unaanza kutetemeka kwa hofu. Na zaidi pale ambapo kila mtu akishalala, machozi huanza kumbubujika na hujifunika shuka gubigubi. Si kwamba Joana ni mwoga kukithiri. Hapana. Joana huona watu usiku. Watu waliokufa, watu wanaotisha na kuogofya! Habari hii ilianzia miaka kumi na mitano huko nyuma kwenye jiji la Berlin, Ujerumani. Joana alikuwa anasoma huko chuo kikuu akichukua fani ya sheria. Alikuwa ni msichana mrembo na mwenye kuvutia kwa namna alivyokuwa anajipangilia nguo, maneno na hata hoja. Alikuwa na marafiki lukuki, lakini zaidi mpenzi wake mwenye asili ya Brazil, akiitwa Moa Santos. Aliyekuwa anampenda na kumheshimu sana. Mara kadhaa Joana alikuwa anaonekana na mpenzi wake huyo wakirandaranda maeneo ya chuo wakishikana ...

PANIELA (SEASON 1) SEHEMU YA 1

Picha
PANIELA SEASON 1 SEHEMU YA KWANZA MTUNZI : PATRICK.CK Ni saa sita za usiku sasa bado jaji Elibariki chukuswa yuko sebuleni akiendelea kupitia kitabu chake cha sheria .Katika meza ndogo kulikuwa na vitabu vingine zaidi ya saba vya sheria.Aliendelea kufungua ukurasa baada ya ukurasa.Alionekana kuwa na mawazo mengi mno.Wakati akiendelea kupitia kurasa za kitabu kile mke wake akaingia pale sebuleni akiwa na kikombe cha kahawa, akakiweka mezani halafu akainama na kumbusu mumewe. “ You need to take a rest now.Tommorow is your big day” akasema Flaviana mwanamke mwenye uzuri wa kipekee.Elibariki akakifunika kitabu chake na kumtazama mkewe ,akachukua kikombe cha kahawa akanywa kidogo na kusema “ Natamani sana nipumzike lakini sina hakika kama nitapata usingizi.” Mke wake akamuangalia kwa makini halafu akasema “ Kuna jambo nataka nikuulize mume wangu” “ Uliza usihofu ” “ Najua kesi hii ni moja kati ya kesi kubwa na ngumu kwako.Hukumu unayotarajia kuitoa kesho inasubiriwa kwa hamu kubwa sana na u...

DIMBWI LA HUBA SEHEMU YA 2

Picha
SIMULIZI: DIMBWI LA HUBA MTUNZI: ALLY MBETU SEHEMU YA PILI Mama yake baada ya kumkosa mchana wakati wa chakula, baada ya kumuona amerudi alimfuata kutaka kujua alikuwa wapi. Alipoingia chumbani alishtuka hali aliyomkuta nayo mwanaye. “Sued mwanangu mbona hivi! Unaumwa?” “Hapana.” “Sasa mbona upo hivyo?” “Basi tu mama natamani kufa.” “Kufa?” “Ndiyo mama.” “Kwa nini?” “Nina imani bila Zulfa siwezi kuishi?” “Zulfa ndiye nani?” “Mwanamke niliyemchagua kuwa mke wangu.” “Sasa huyu Zulfa kafanya nini?” “Nimeambiwa anataka kwenda nje kusoma.” “Sasa tatizo nini?” “Sicho tulichokipanga, mzee wake ana roho mbaya aliona kumuoa mwanaye ningefaidi.” “Huyo Zulfa anakaa wapi?” “Kayenzo.” “Kayenzo, mtoto wa nani?” “Kipepeo.” “Yule tajiri wa Kayenzo?” “Ndiyo mama.” “Mwanangu mbona unataka mazito, kwanza baba yako akisikia unafikiri kutakuwa na usalama? Unataka kumchokoza baba yako? Kwanza mapenzi umeyaanza lini mpaka kufikia hatua ya kupanga na ndoa wakati huna kazi wala chumba.” “Ningejua nitamuweka wa...

JINI WA DARAJA LA SALENDA SEHEMU YA 2

Picha
SIMULIZI: JINI WA DARAJA LA SALENDA MTUNZI: ALLY MBETU SEHEMU YA PILI ILIPOISHIA ; Kingine, hali waliyomkutanayo kama mtu aliyekuwa amefariki dunia na kushangazwa na jinsi alivyoamka na kukutwa hana ugonjwa wowote zaidi ya uchovu wa usingizi. Alijiuliza hali ile imemtokea kwa sababu gani. Akiwa katika dimbwi la mawazo shoga yake kipenzi, Sharifa aliingia. “Vipi shoga mbona leo sikusomi?” “Mmh, shoga wee acha tu kuna mambo yamenitokea yananichanganya.” “Yapi? Hebu kaa chini nikueleze yaliyonisibu najuta kwenda klabu usiku.” “Yapi tena hayo shoga?” Suzana alimueleza yote aliyokutana nayo usiku na hali iliyomkuta baada ya kumaliza kuoga ili aende kanisani na alipoamka na kukukuta watu wamemzunguka na kumueleza walimkuta akiwa kama amekufa. “Haa! Shoga unayosema ni kweli?” “Kweli kabisa.” “Huyo mtu unasema umemuona wapi?” “Daraja la Salenda” “Mmh!” Sharifa aliguna. “Mbona unaguna?” “Mbona tukio linafanana na kama langu.” SASA ENDELEA... “Lako?” “Eeeh.” “Tukio gani?” “Unajua kuna mtu nilimu...

SHAIDA SEHEMU YA 2

Picha
SIMULIZI: SHAIDA MTUNZI: AISHA KHAN SEHEMU YA PILI TULIPOISHIA: "We Aisha nakuheshimu" Ndende alimnyooshea kidole ishara anaweza kumfanyia chochote kibaya. "Weeee!!! Subutu nikusambaze muda huu, au umesahau nilivyokua na kukunguta utotoni" "Nini kinaendelea?" ilikuwa ni swali kutoka kwa baba yake Ndende ambae alifika muda huo. SONGA NAYO Wote kwa uoga waligeuka kumtazama bila kujua watamjibu nini ili kujitetea. "Tutazidi jamani" Aisha aliwaaga baada ya kuona kizazaa kimeingilia kati, ila baba yake Ndende alimsimamisha akisema. "Nauliza tena nini kinaendelea?" baba yake Ndende alionekana kutaka kujua kiundani ila wote wakakaa kimya kuashilia hakuna kilichotokea. Siku zilisonga ndoa ya Eddy na Shaida ilifungwa, wakaishi kama mke na mume jambo ambalo Eddy alilitamani kwa muda murefu licha alikuwa hajui kama kweli anampenda Shaida ama anapenda tendo la ndoa, ingawa Shaida aliamini mia mia kuwa anapendwa na atadumu kwenye ndoa yake. Maisha y...

MIMBA YA JINI SEHEMU YA 5

Picha
MIMBA YA JINI 05 ILIPOISHIA: �Niliwaambia mfanye mapenzi saa ngapi?� �Saa nne.� �Ndiyo muda uliofanya?� �Hapana lakini haikuvuka sana.� �Mustafa niliwaeleza saa nne kamili lakini mmevuka muda kwa nini umepuuza maagizo yangu?� �Samahani kwa hilo.� SASA ENDELEA.. � Mmh! Sijui...halafu kwa nini hukufurahia uamuzi wa mkeo?� �Nimefurahi ndiyo maana tumekubaliana kutanguliza mtoto wa kike.� �Si kweli Mustafa, moyoni hujafurahia uamuzi wa mkeo kwa kulazimisha kutangulia mtoto wa kike kitu kitakachompa matatizo mtoto atakayezaliwa.� �Kwa nini?� Mustafa alishtuka. �Kuukunja moyo wako wakati wa tendo la ndoa tofauti na siku zote. Mimba iliyoingia umeitia sumu.� �Sumu?� Mustafa alishtuka. �Ndiyo, ili kuiondoa unatakiwa kuukunjua moyo wako bila hivyo mtoto atakuwa na matatizo.� �Nimekuelewa.� �Basi mi nikuache ufanye kazi.� �Nashukuru ila nilikuwa na hamu sana ya kuonana na wewe.� �Usiwe na wasi Mustafa utaniona mpaka utanichoka kwanza tumalize tatizo linalowakosesha raha kwa muda mrefu.� �Asante...

ADUI WA MAISHA SEHEMU YA 5

Picha
SIMULIZI: ADUI WA MAISHA MTUNZI: LISSA WA MARIAM SEHEMU YA TANO Baada ya kutoka hospital Isabella alifanya taratibu za kwenda mwanza, baadhi ya wanafunzi na walimu walimchangia rambirambi, Lameck nae hakumuacha pekee yake, kama alivyoahidi alitoa kiasi cha pesa kwenye akaunti yake wakasafiri wote pamoja na baadhi ya wanafunzi, baada ya kufika mwanza Lameck alimtaarifu mama yake kuwa yupo mwanza "Umeenda kufanya nini mbona gafla" Mama Lameck aliuliza "Kuna rafiki yangu kafiwa na wazazi wake wote wawil" "Jamani dah!! Mpe pole sasa wakimaliza mazishi si unarudi" "Ndio mama" "Haya kuwa makini" waliagana na kukata cmu, msiba ukaisha na baadhi ya wanafunzi wakarudi Dar, ni Lameck pekee ndie Alibaki alisubiri mpaka 40 iishe ndipo arudi, mapenzi aliyokuwa nayo kwa Isabella yalizidi Mara mbili, siku zikapita hatimae wiki ya pili ikawa inakaribia, mama yake alikasirika na kumpigia simu "Hivi wewe upo kwa nani huko mwanza na huku chuo umemuac...