ANGA LA WASHENZI SEHEMU YA 1



ANGA LA WASHENZI -- 001

Simulizi_za_series

Mvua ilikuwa inanyesha sana. Hali ya hewa ilikuwa baridi ikiambatana na upepo wa wastani. Watu wengi hawakwenda kazini, na hata wanafunzi pia wakitega shule kwa kisingizio cha barabara kufurika maji.
.
.
.
Pengine watu hawa walikuwa na hoja kutokana na miundombinu dhaifu ya jiji la Dar es Salaam ambayo haiwezi kurandana na mikikimikiki ya mvua. Ila kwa mwanaume Jonathan Mchau, hilo halikuwa na mashiko kamili kwani yeye alikuwa ofisini akiendelea na kazi zake kama ilivyo ada.
.
.
.
Ni ndani ya chumba kidogo kinachopatikana maeneo ya mwenge. Kwenye kuta za chumba hicho kulikuwa kumetundikwa picha kadhaa za kuchorwa kwa mikono. Picha hizi zilikuwa zimeundwa kimafumbo lakini pia zikibeba utajiri wa tamaduni za Afrika kwa ujumla.
.
.
.
Kama ungelipata nafasi ya kutembelea hapo basi ungepatwa na kamshangao kidogo kutazama picha hizo zilizofumwa na rangi mbalimbali za kuvutia kiasi kwamba ukasahau kuwa eneo hilo limepakana na barabara yenye makelele lukuki ya magari. Na hata kuta za jengo hilo zina nyufa kadhaa.
.
.
.
Mwanaume huyu ajulikanaye kwa jina la Jonathan, joh, ama Jona kama wamuitavyo watu wa karibu, alikuwa ni mwanaume mweusi mtulivu mwenye mwili wa kujaa, macho makubwa mabovu yasaidiwayo na vioo vya miwani, nywele ndefu kichwani na ndevu alizozichonga umbo la 'o'.
.
.
.
Hakuwa mtanashati sana, pengine kwasababu alikuwa kazini na kazi yake aihitaji unadhifu wa hali juu ilhali unacheza na rangi. Ila alikuwa mtulivu sana, na macho yake yaliganda kwenye karatasi aichorayo kwa umakini wa hali ya juu.
.
.
.
Alikuwa ndani ya ulimwengu wa peke yake asijali kabisa yanayoendelea nje ya karatasi. Unaweza kudhani mwanaume huyu hakuwa anajua kama kuna mvua ilikuwa inanyesha. Umaanani huu kupita kiasi ukamfanya asifahamu kama kuna mgeni ameingia eneo lake na kusimama kwa sekunde kadhaa.
.
.
.
Akashtuliwa, "Hello!"
.
.
.
Akatazama na kumkuta mwanamke fulani mrembo, mrefu mwenye rangi maji ya kunde. Alikuwa amevalia sweta rangi ya kijivu iliyofunika blauzi yake nyeupe, pamoja na suruali ya jeans iliyobana vema umbo lake la figa. Miguuni alivalia raba nyekundu.
.
.
.
Nywele na masikio yake alikuwa ameyaziba kwa kofia kubwa jeusi la soksi. Mgongoni alikuwa amebebelea begi kubwa jeusi, haya ya kuhifadhia tarakilishi mpakato. Uso wake ulikuwa mfupi na mpole. Macho yake yalikuwa ya wastani ila makali. Mdomo wake mdogo alioupaka rangi ya kahawia ulichanua kwa tabasamu.
.
.
.
"Samahani kwa kukutoa kazini," akasema mwanamke kwa sauti ya kumlaghai nyoka.
.
.
"Usijali," akadakia Jonathan, "karibu sana." Akaacha kazi akasimama kumlaki mgeni.
"Ahsante. Hapa ndiyo kwa Joh?"
"Yes, ndiyo hapa."
"Na wewe ndiye Joh mwenyewe?"
"Ndio, ni mimi."
"Ook, nimeagizwa na Beatrice Shauri kuulizia mzigo wake."
"Bite?"
"Ndio!"
.
.
.
Jonathan akatabasamu. Akafuata mfuko mmoja mkubwa mweupe wa rambo, ndani yake ulikuwa na kitu cha umbo la mstatili, akaunyanyua na kumkabidhi mgeni.
.
.
.
"Unaweza ukatazama."
.
.
.
Mgeni akatazama mzigo huo kisha akaurudisha ndani ya mfuko.
.
.
.
"Ahsante sana. Unamdai?"
"Hapana."
"So naweza nikaondoka nao?"
"Hapana." Jonathan akatikisa kichwa. "Siwezi nikakupatia maana sijapata ridhaa ya mmiliki."
"Bite ni dada yangu."
"Taarifa hiyo haijitoshelezi kukupa mzigo wake, dada. Hakunipa agizo hilo."
.
.
.
Mwanamke yule akaguna na kubinua mdomo. Akapandisha mabega na kuzungusha macho.
.
.
.
"Ok," akasema kwa kupitia puani kisha akaenda zake. Ila punde anarejea tena.
"Kaka mbona unakuwa si mwelewa lakini?" Alilalama. Macho yake yalikuwa yamelegea, mdomo wake ukitepeta.
"Nimekwambia Bite ni dada yangu, ameniagiza. Simu yangu imezima chaji unajua umeme unavyosumbua siku hizi, ningempigia uongee naye!"
.
.
.
Joh alipigwa na bumbuwazi. Kuna kitu alikikokotoa kichwani.
.
.
.
"Dada," akaita. "Siwezi nikakupa kazi ya mtu. Na hii ni kwasababu sikupewa agizo hilo. Ni swala la uaminifu tu. Sikufahamu, siwezi kukuamini namna hiyo."
.
.
.
"Basi ntakuongezea pesa mara mbili ya aliyokulipa Bite," akasema mwanamke huyo kwa kujiamini. Hapo sasa ndiyo Jonathan akapata wasiwasi zaidi. Kwanini mwanamke huyu anataka mzigo huu kiasi hiki?
.
.
.
Aliona haja kubwa ya mwanamke huyo ndani ya macho yake. Alikuwa anataka ule mzigo kwa hali na mali.
"Sema basi," mwanamke akasisitiza. Uso wake ulikuwa umekunjana. Alitazama majira ya saa yake kana kwamba mwanafunzi aliyechelewa zamu ya mwalimu mnoko.
"Unataka shilingi ngapi?" Akauliza.
"Sitaki pesa yako," Jonathan akajibu na kuongezea: "Naomba uende, dada."
.
.
.
Mwanamke akashusha pumzi ndefu. Akavua begi lake na kuzamisha mkono wake wa kuume ndani. Jonathan akapata shaka. Alitazama mkono huo vema. Alidhani huenda ukatoa silaha.
.
.
.
Kabla mkono huo haujatoka ndani ya begi, sauti ya wanaume ikasikika. Jonathan na mgeni wake wakatazama sauti hiyo inapotokea. Mlangoni wakawaona wanaume wawili waliovalia makoti marefu meusi ya kuwakinga na mvua.
.
.
.
Wanaume hawa walikuwa warefu na weusi. Mmoja alikuwa na mustachi mnene, mwingine kidevu na mashavu yake yakiwa hayana harara za ndevu. Miili yao ilikuwa imejaa wakitembea kikakamavu.
.
.
.
Haikuchukua muda mrefu Jonathan akagundua wanaume hao walikuwa ni wana usalama. Kwa namna walivyokuwa wanaongea, kutembea na muonekano wao pia ulisadifu hiyo dhana.
.
.
.
Alirudisha macho yake kwa yule mwanamke, akaona mwanamke huyo akifunga begi lake na huku mkononi akiwa mtupu. Mwanamke akamtazama Jonathan kwa jicho baya kisha akaondoka zake akisonya.
.
.
.
Jonathan alimsindikiza mwanamke huyo mpaka alipotoka mlangoni, kisha akahamishia macho yake kwa wageni wapya.
.
.
.
"Karibuni."
"Ahsante," aliitikia mwanamume mmoja kisha kwa pamoja wakamsalimu Jonathan.
"We ni Jonathan Mchau?" Aliuliza mwanaume mwenye mustachi. Sauti yake ilikuwa ya madaraka. Walikuwa wanamtazama Jonathan kana kwamba wanamfananisha na mtu waliyemuona kitambo.
"Ndiye mimi," Jonathan akajibu.
.
.
.
Leo ilikuwa ni siku ya tofauti sana kwa Jonathan. Ugeni wa pili sasa huu unamtembelea. Kazi iliyomfanya asijali hali ya hewa akaja ofisini, ilikuwa imesimama. 'Karoho' kalikuwa kanamuuma. Aliona anapoteza muda.
.
.
.
"Tuna maongezi kidogo na wewe," akasema mwanaume mwenye mustachi. Yeye ndiye alikuwa muongeaji mkubwa mwenzake akiwa kimya.
"Karibuni," Jonathan akasema akinyooshea mikono yake ndani.
"Tunaweza tukafanyia hayo maongezi kwenye gari?"
"Kwenye gari!" Jonathan alistaajabu. "Ni maongezi gani hayo? Na nyie ni wakina nani? - hamjajitambulisha."
"Sisi ni polisi." Wanaume wale wageni wakaonyeshea vitambulisho vyao. "Hivyo usijali."
"Sijali, ila ningependekeza tufanyie hayo maongezi hapa hapa ofisini kwangu," Jonathan alisema akiketi kitako.
Wanaume wale wawili wakatazamana kisha muongeaji akasema:
"Sawa."
.
.
.
Wakavuta viti vilivyoko kando, walionyeshewa na Jonathan, wakaketi.
.
.
.
"Jonathan, sisi sio wakaaji sana. Kwa majina naitwa inspekta Norbet Mlanje na huyu mwenzangu ni inspekta Nombo tumetokea kituo kikuu, central."
"Karibuni inspekta."
"Ahsante kwa mara nyingine. Nadhani mpaka hapo utakuwa ushajua tumekuja kufanya nini."
"Sijajua," Jona akasema akitikisa kichwa.
"Sawa, si mbaya tukaliweka wazi," akasema Inspekta Norbet akikuna ndevu. "Kama tulivyosema hapo awali, tumetoka central, na tumeagizwa kuja hapa kwa ajili ya kukuomba kurejea kundini. Mkuu anakuhitaji sana."
.
.
.
Jona akatabasamu.
.
.
.
"Siwezi kurudi," akajibu kwa ufupi na kisha akasimama. "Nina kazi nyingi zinaningoja. Mnaweza mkanipa nafasi?"
.
.
.
Inspekta wakatazamana alafu wakanyanyuka kishingo upande.
.
.
.
"Jona," inspekta Norbet aliita. "Taifa lako linakuhitaji kwa sasa. Nadhani ni wakati wa wewe kuacha ukaidi na kusikiza wito huu."
"Inspekta Norbet," Jona akaita. "Sihitaji kazi yenu, naomba umwambie mkuu hilo. Tena umsisitizie. Sihitaji kazi yenu hata kidogo."
.
.
.
Inspekta wakatazamana kwa macho ya paka.
.
.
.
"Sawa, ila utakapobadili mawazo yako usisite kututaarifu."
.
.
.
Jonathan hakujibu, inspekta wakaondoka. Walifika mlangoni Norbet akamtazama tena Joh kana kwamba mama aliyekata tamaa juu ya mwanaye. Kisha wakatokomea.
.
.
.
Jonathan alitafakari kwa dakika mbili, akaketi kuendelea na kazi yake aliyokuwa anaifanya hapo awali. Ila kwa sasa akili yake haikuwa imetulia. Mawazo yalimpoka atensheni. Alimfikiria yule mwanamke, alafu pia na wale inspekta. Alijikuta anakosea kutenda kazi kila mara.
.
.
.
Mwishowe aliacha, akasimama na kwenda nje kutazama madhari, pengine angechangamsha akiliye. Alitazama namna mvua inavyokita ardhi, barabara ilivyolowana. Alitazama jinsi matairi ya magari yanavyotapanya maji barabarani.
.
.
.
Alitazama anga lilivyojibana na kuwa jeusi. Namna palivyokuwa tulivu usidhanie kama hapo ni Dar, tena majira hayo.
.
.
.
Akiwa anarandisha macho yake mithili ya mtalii mbugani Serengeti, kuna kitu alikiona kikamvutia. Mara ya kwanza alikipuuzia, na hata ya pili pia. Mara hii ya tatu akaamua kukitilia maanani. Ilikuwa ni gari kubwa, Range Rover Sport nyeusi, lililosimama hatua ishirini na tano za mtu mzima toka kwenye banda lake.
.
.
.
Taa za nyuma za gari hilo zilikuwa zinawaka. Gari lilikuwa linachemka, ungeliona hilo kwa wepesi kwa kutazama bomba lake la kutolea moshi. Pleti namba ya Kenya. Vioo vyake vilikuwa vyeusi, hivyo hata kama ungekuwa karibu usingeona walio ndani.
.
.
.
Jona alilitazama gari hilo akijiuliza maswali mepesi kichwani. Lipo hapo tangu muda gani? Linafanya nini hapo? Mbona haliondoki? Linamsubiri nani ama nini ilhali mabanda yamefungwa? Mara gari hilo linatiwa moto na kuondoka. Jona analisindikiza likiyoyoma kisha anarudi zake ndani kuendelea na kazi. Angalau akili yake ilikuwa freshi.
.
.
.
Alidumu kazini mpaka majira ya jioni akiwa ameisogeza sana kazi yake. Alifunga banda kwenye majira ya saa kumi na mbili, akapanda bodaboda mpaka kwenye baa moja isiyo na jina, maeneo ya karibu na makazi yake, Mbezi beach GOIG. Hapo akatulia akiwa ameagizia Alvaro baridi.
.
.
.
Watu walikuwa wachache, bila shaka sababu ya hali ya hewa. Jona alijitenga mbali na watu, akiketi kwenye meza pweke. Macho yake yalikuwa yanachambua mazingira huku mdomo wake ukipiga mafundo kadhaa ya kinywaji.
.
.
.
Taratibu akiwa hapo, anamezwa na tafakuri na taswira mithili ya ndoto. Haikuchukua muda mwingi kuhamishwa toka kwenye fahamu zake mpaka ulimwengu huo mwingine.
.
.
.
Hii ndiyo sababu mwanaume Jona hapendi kuketi pasipo shughuli. Kila anapokuwa huru, akili yake humkumbusha yaliyopita. Na yaliyopita si mema. Humuumiza. Humtonesha kidonda sugu kisichotaka kupona.
.
.
.
Anajiona kwenye nyumba kubwa inayoungua moto. Anavuja jasho jingi akitoa macho huku na kule. Anaita jina lisilosikika. Anazunguka huku na kule. Mbao za paa zinaanguka. Hewa inakuwa nzito ndani ya nyumba anashindwa kuhema. Macho yake yanamwaga machozi. Anajikuta anaishiwa nguvu akikohoa kwa pupa. 
.
.
.
Haraka anatoka ndani. Anatembea hatua kadhaa kuacha kibaraza, mara anaanguka chini. Anajitahidi sana kuhema. Jasho bado linaendelea kummiminika. Punde fahamu zinaacha mwili wake, anazirai. 
.
.
.
“Kaka!” kwa mbali sauti ya kike ilipenya kwenye ngoma ya masikio ya Jona.
“Kakaa!” sauti hiyo ikajirudia, mara hii kwanguvu ikiambatana na kupigwa kwa meza. Jona akashtuka. Mbele yake alikuwa amesimama mhudumu, mwanamke mtu mzima mwenye uweupe mwekundu wa kujichubua.
.


ITAENDELEA........



TUPATIE NYOTA 5 KWENYE APP YETU KULE PLAY STORE NA KU COMMENT ILI TUPATE SUPPORT YAKO.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: BINAMU 🔞 SEHEMU YA 11

KIJIJINI KWA BIBI SEHEMU YA 1-5

CHOMBEZO: MASSAGE ROOM🔞 SEHEMU YA 21