Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2022

MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN SEHEMU YA 1

Picha
MKUFU WA MALKIA WA GOSHEN -- 001 *Simulizi za series* Jua lilinyanyuka na kuangaza ardhi ya Goshen: mojawapo ya tawala kubwa iliyopata kutokea mashariki ya mbali katika karne ya kumi baada ya kuzaliwa kwa kristo. Ndege wake wakubwa wenye rangi za kuvutia waliamka wakaruka huku na kule wakitandaza sauti zao nyembamba. Sauti hizo marigoli zikawasili masikioni mwa malkia Sandarus na kumwamsha. Alikuwa amevalia nguo nyepesi za kulalia zilizokuwa zinaangaza kuonyesha mwili wake mchanga wa miaka ishirini na tano. Kichwa chake chenye hekima kilikuwa kimefunikwa na nywele nyingi rangi ya kahawia. Miguu yake mirefu ila yenye nyama ilisimika ardhini na kusimamisha mwili wake mrefu mwembamba. Alah! Alikuwa mzuri haswa. Macho yake yalikuwa makubwa yaliyolegea. Mdomo wake ulikuwa mdogo ila hakika ukichanua kwa tabasamu ungekufanya uache shughuli yako na kumtazama. Nyonga zake zilijiachanua na kukikimbia kiuno. Vidole vyake vilikuwa vyembamba virefu vyenye kucha bawabu. Tumbo lake flati na mapaja me...

BEYOND PAIN SEHEMU YA 1

Picha
BEYOND PAIN SEHEMU YA 1 MTUNZI : PATRICK .CK Ni saa kumi jioni nikiwa maeneo ya Kimandolu nikielekea Usa river katika baa iliyotulia ya Roterdam garden mahala panapofanyika vikao vya harusi yangu.Wanakamati ya maandalizi walichagua mahala hapa kutokana na utulivu wake kwani kuna bustani nzuri na hata huduma zake ni nzuri sana.Nikiwa maeneo haya ya Kimandolu gari ikienda taratibu kutokana na magari mengi kukaa pembeni ya bara bara kwa muda mrefu kwa kupisha misafara ya viongozi wa jumuia ya Afrika mashariki waliokuwa na kikao chao hapa Arusha.Siku zote kunapokuwa na mikutano ya namna hii jijini Arusha huwa kunakuwa na adha kubwa kwa watumiaji wa bara bara hii ya Moshi - Arusha kwa sababu ndiyo bara bara kuu waitumiayo viongozi hawa wakitokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).Mara simu yangu ikaita nikaitazama na kukuta ni Mr Cheleo mmoja kati ya wanakamati. ?Haloo kaka? nikasema ?Haloo ,uko wapi? Sisi tumeshafika tunakusubiri wewe tu.? ?Niko njiani kaka si unajua ...

MWANAMKE JINI SEHEMU YA 1

Picha
MWANAMKE JINI SEHEMU YA 1 MTUNZI: FAKI A FAKI Sitausahau mwaka 1978. Nina sababu tatu za kutousahau mwaka huo. Sababu ya kwanza ni kuwa kulitokea vita vya Kagera. Majeshi ya Iddi Amin aliyekuwa Rais wa Uganda yalivamia nchi yetu na kusababisha maafa makubwa. Kaka yangu wa kwanza alikuwa ni miongoni mwa askari waliokuwa mstari wa mbele waliokwenda kuikomboa nchi yetu na aliuawa katika vita hivyo. Sababu ya pili ya kutousahau mwaka huo ni kuwa ndio mwaka nilioanza kufanya kazi. Niliajiriwa na kampuni ya STC iliyokuwa na maduka ya ushirika nchi nzima. Na mwaka huo pia ndio nilitimiza umri wa miaka ishirini. Lakini sababu ya tatu na iliyokuwa kubwa zaidi ya kutousahau mwaka huo ni kuwa nilikutana na tukio ambalo lilibadili maisha yangu. Je lilikuwa tukio gani? SASA ENDELEA Ilikuwa februari 18 mwaka 1978. Nilikuwa mmoja wa wafanyakazi wa STC tuliokopeshwa pilipiki. Furaha yangu ikanituma kwenda kuangalia sinema. Wakati huo hakukuwa na video wala televisheni. Kulikuwa na majumba ya sinema. K...

PENZI LISILO NA MWISHO SEHEMU YA 2

Picha
Simulizi: PENZI LISILO NA MWISHO Mtunzi: NYEMO CHILONGANI SEHEMU YA 2 ILIPOISHIA “Wakina nani?” ilisikika sauti ya msichana mmoja, ikamfanya Razak kuogopa, akageuka kule sauti ilipotoka, akanyoosha bunduki kuelekea kule. “Unataka kuniua?” ilisikika sauti hiyo ikiuliza. “Wewe ni nani?” aliuliza Razak huku kwa mbali akitetemeka..... ENDELEA alihisi kama alikutana na jini kutokana na muda na mahali penyewe. “Naitwa Aisha...” “Aisha wa wapi?” “Wa hapahapa...” “Unataka nini?” “Kwani wewe unataka kuwaua wakina nani?” “Wewe nani?” “Kwani nimekwambia mimi nani?” Muda wote Razak alikuwa akitetemeka, japokuwa alikuwa pembezoni mwa bahari hivyo na upepo mwingi kupuliza lakini kitu cha ajabu kijasho chembamba kikaanza kumtoka. Alitetemeka, alihofia, moyo wake ulimwambia kwamba yule aliyesimama mbele yake hakuwa binadamu bali alikuwa jini ambalo kazi yake ilikuwa ni kukaa pembezoni mwa bahari kwa ajili ya kufanya mawindo yake. Msichana yule alisimama sehemu iliyokuwa na giza, Razak hakuweza kumuona...

JINA LA URITHI SEHEMU YA 2

Picha
Simulizi : Jina La Urithi Sehemu Ya Pili (2) kule nyumbani Njile,,maisha yaliendelea,lakini mtoto Laula aliendelea kufanya matukio ya ajabu,,,habari zikazagaa kila kona ya kijiji,,kuwa Laula si binadamu wa kawaida.... mkuu wa kijiji hicho,akaamuru Njile pamoja na mtoto wake wafukuzwe,,wasiendelee kuishi katika kijiji hicho.. Njile hakuwa na namna,,akalazimika kuuza kila kitu kilichokuwa ndani ya nyumba,,pamoja na nyumba yenyewe ,,,lakini hakuna mtu aliyejitokeza kununua hata kitu kimoja,,hakuna aliyetamani hata kupewa kitu bure..Njile akaamuaa kuondoka na mwanae Laula,, akaelekea mjini,,ni mbali na kijiji hicho! Maisha ya Njile yakawa magumu kupita kiasi,,wakati mwingine hakuweza kupata mlo siku nzima,, Laula akashindwa kuendelea na masomo,,Njile akafanya jitihada za kutafuta vibarua ilimradi apate pesa ya kumpatia mlo mwanae Laula,, siku zilizidi kusonga,,wakiwa wanalala nje,,kitendo hicho kilimuumiza sana Laula. lakini hakuna namna. siku moja nyakati za usiku,,Njile aliugua ghafla,,h...

UNA NINI LAKINI MELISSA? SEHEMU YA 2

Picha
* UNA NINI LAKINI MELISSA? -- 02* *Simulizi za series* ILIPOISHIA Mama akatoa macho kwa mshangao. “Hapana!” akakanusha akitikisa kichwa. “Hapana, mpenzi. Ni hatari!” “Huoni ni hatari akiendelea kutokujua?” Baba akauliza. Mama akatazama chini akiwa na sura ilonywea. Alikuwa anahofia. Alikuwa anatakiwa kuhofia. ENDELEA Hakusema jambo mpaka pale Baba alipomshika bega na kumwambia kwa upole, “nikamwambie? Niruhusu nifanye hivyo!” Mama akatikisa kichwa. “Hapana, Gerald. Si muda sahihi hivi sasa. Ni mapema sana. Tungoje kidogo tafadhali.” Baba akamtazama asiseme jambo b ali kushusha pumzi ndefu puani na kisha akajiendea zak e ajiandae kuoga. Muda si mrefu, Darren akaaga anakwenda. Mama akamwomba sana ile picha ya Bibi lakini Darren akagoma kumpatia. Kwa kumpoza akamwambia kuwa atamrudishia kesho kutwa yake. “Nakuahidi mama,” Darren akaapa kabla hajaenda zake. Alinyookea nyumbani kwake kisha akampigia simu Melissa akimwomba aje nyumbani kwake kwani kuna dharura. Kama baada ya...

DEAR EX SEHEMU YA 4

Picha
STORY DEAR EX MTUNZI : MADAM YUSTAR SEHEMU YA NNE Tuendeleee.... Doreen alishtuka saana baada ya kuona Peter ndo Mc, alimuomba Mwenyezi Mungu apuepushie na chochote kile alichokipanga Peter. Heka heka za sherehe zilianza, kila mmoja alikuwa na furaha lakini Doreen uso wake ulijawa na tabasamu lenye uchungu ndani yake. Hakujua kwanini Peter anafanya hayo yote. Utambulisho ulikamilika , watu walikula na kukata keki. Hatimae maharusi walipewa zawadi za kutosha. John mda wote alitabasamu kwa furaha huku akimwangalia mke wake. Wakati shamra shamra zinaendelea, MC alitangaza kupokea zawadi ambayo iliitajika kusomwa pale mbele, bila kipingamizo John aliruhusu ujumbe usomwe. Ujumbe uliandikwa hivi; "Naelewa nipo mbali na wewe, umbali wangu mimi na wewe umekufanya ukaolewa bila kujali hisia zangu. Doreen nimekuwa nikikukumbuka sana hasa nyakati za huzume. Nakumbuka ulikuwa mwanamke unayebeba matatizo yangu kama yako. Huenda nisiwe na zawadi yoyote kwako lakini nakiri kutoka moyoni,...

BINTI MFALME SEHEMU YA 3

Picha
HADITHI- BINTI MFALME SEHEMU - 3 MTUNZI- LISSA WA MARIAM "Nitafanya chochote ikiwezekana tutapambana, huyo mtu wanayemtaka wana Bweleo lazima afe, itabidi vijana wangu wasikae bure wawe wanafanya mazoezi kwaajili ya pambano, maana muda wowote naweza kufanya jambo kubwa" "Vizuri sana mfalme wangu, mimi nakuunga mkono, alafu kwanini usiongeze wanaume mashujaa waweze kufanya? kuna kijana mmoja niliwahi kumshuhudia akipambana, hakika ungemuweka hapa lingekuwa jambo bora, huenda akakusaidia katika mipango yako" "Asante sana malkia wangu, kama itawezekana niitiwe huyo kijana nimuone niweze kuongea nae" mfalme alisema ********* Siku ya pili Chansa aliitwa kwa mfalme na kuweza kuongea nae "Nimepata sifa zako kuwa wewe ni kijana shupavu, nataka nikupatie kazi, ila bado sijaona ushupavu wako, unaweza kunithibitishia?" Mfalme alimuuliza "Ewe mfalme wangu mtukufu, niambie chochote nitakifanya" Chansa alijibu kwa kujiamini "Nataka upigane na wa...

MZIMU UMERUDI TENA EPISODE:8

Picha
MZIMU UMERUDI TENA EPISODE:8 MTUNZI:HAMIDU MCHAKO ..............ILIPOISHIA......................... Niliwastua wenzangu kua turudi kambini kunatatizo limetokea. Tulianza kurudi ila sikua na hakika kama tutawahi kufika maana yalikua ni masafa marefu hadi kufika ................ENDELEA................. Safari ya kurudi iliendelea tulizidi kukaza mwendo ila kwa kua sikuile ilikua ni ya mkosi basi hata safariyetu ilikua hivyo hivyo. Tulipoondoka pale mawindoni tuli muua mtoto wa simba hivyo kulikua na simba mmoja dume alichukia kitendo kile. Baada ya kuona tunaondoka nae aliunga msafara bila sisi kujua. Tukiwa bado tuko njiani tukiwa na kasi ya ajabu simba yule dume alianza kutushamburia taratibu. Mwanzo mimi nilihisi kama vile kunakitu kisichokua cha kawaida kimetokea nyuma ya msafara wetu. Lakini nilipuuzia na hapo ndipo nilipofanya kosa. Tukiwa tunaendelea na safari maskio yangu yalicheza yakiashiria kunatatizo limetokea kwenye msafara wetu.Lakini pia nilipuuzia Akili yangu fikra yangu ...