UNA NINI LAKINI MELISSA? SEHEMU YA 2



*UNA NINI LAKINI MELISSA? --

02*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Mama akatoa macho kwa mshangao. “Hapana!” akakanusha akitikisa kichwa. “Hapana, mpenzi. Ni hatari!”

“Huoni ni hatari akiendelea kutokujua?” Baba akauliza. Mama akatazama chini akiwa na sura ilonywea. Alikuwa anahofia.

Alikuwa anatakiwa kuhofia.

ENDELEA
Hakusema jambo mpaka pale Baba alipomshika bega na kumwambia kwa upole, “nikamwambie? Niruhusu nifanye hivyo!”
Mama akatikisa kichwa. “Hapana, Gerald. Si muda sahihi hivi sasa. Ni mapema sana. Tungoje kidogo tafadhali.”
Baba akamtazama asiseme jambo b ali kushusha pumzi ndefu puani na kisha akajiendea zak e ajiandae kuoga. Muda si mrefu, Darren akaaga anakwenda. Mama akamwomba sana ile picha ya Bibi lakini Darren akagoma kumpatia. Kwa kumpoza akamwambia kuwa atamrudishia kesho kutwa yake.
“Nakuahidi mama,” Darren akaapa kabla hajaenda zake. Alinyookea nyumbani kwake kisha akampigia simu Melissa akimwomba aje nyumbani kwake kwani kuna dharura.
Kama baada ya lisaa, Melissa akawa amefika hapo. Alikuwa amevalia topu nyeupe na jeans nyeusi. Alipendeza. Tuseme hata akivalia gunia mwanamke huyu hupendeza kutokana na umbo na uzuri wake.
Akamkumbatia Darren na kisha akamjulia hali kwa tabasamu pana. Lakini akafanikiwa kuona jambo usoni mwa Darren. Mwanaume huyo hakuwa sawa.
“Kuna tatizo Darren?” akauliza kwa sauti yake ya chini.
Darren ndipo akatoa picha ile, picha ya Bibi yake na wale wenza, na kumwonyeshea Melissa. “Melissa huyu ni wewe?”
Kwa mwanzoni Melissa akapigwa na butwaa. Mtu alikuwa akifanana naye vilivyo. Ilikuwa ni ajabu. Akachukua kama dakika mbili akitazama picha ile kisha akamuuliza Darren, “umetoa wapi picha hii?”
“Kwa Bibi yangu,” Darren akajibu. “Yule niliyekuambia kumhusu.”
“Yule marehemu?” Melissa akauliza upesi. Brian akatikisa kichwa. “ Ndiye huyo huyo!”
“Na yeye ni yupi kati ya hawa?” 
“Huyu hapa!” Darren akaonyeshea kwa kidole. “Hapa ni mnamo miaka ya alfu moja mia tisa na hamsini!”
Melissa akaendelea kuitazama ile picha kana kwamba mtu anayekumbuka jambo. Darren akamuuliza, “Vipi Melissa? Umemtambua huyo mtu?”
Melissa akatikisa kichwa akiendelea kutazama ile picha alafu nwishowe akairejesha mikononi mwa Darren na kusema, “Anafanana na mimi sana!”
“Ndio! Hata mimi nilishangazwa sana ndiyo maana nikaibeba nije nikwonyeshe!”
Melissa akawa amenyamaza kimya. Macho yake yalionyesha yu mbali kifikra. Darren akamtazama na kumwita mara mbili kabla mwanamke huyo hajashtuka na swali, “Unaweza ukanipeleka huko kwa Bibi yako?”
“Amefariki!” Darren akamjibu akimtolea macho. “Au wataka kuona kaburi?”
“Twende hivyo hivyo!” Melissa akasihi. “Sidhani kama kutakuwa na shida, Darren!”
Darren akafikiri kidogo kisha akamwambia wataenda huko mwisho wa wiki kwani atabanwa na kazi hapa siku za usoni.
“Darren,” Melissa akaita akijitengenezea kumtazama mwanaume huyo. “Naomba, nipo chini ya miguu yako, tafuta siku ya karibuni. Mpaka mwisho mwingine wa wiki ni mbali sana!”
Darren akashangazwa na hitaji hilo la ghafla. “Melissa, ni haraka mno! Vipi kuhusu rat—”
“Tafadhali, Darren!” Melissa akanong’ona kwa huruma. Macho yake yalipoa na uso wake ukiwa kama ule wa mtoto aombapo kitu. Darren akashindwa kukataa. “Sawa, basi tufanye keshokutwa.”
“Kwanini sio kesho?” Melissa akauliza kwa upole. Darren akamtazama kwanza mwanamke huyo, alafu punde uso wake ukawa mgumu, “Melissa kwani kuna nini huko kitakachopotea tukikawia?”
“Darren, ungalikuwa wewe umefanana na mtu pichani hivi usingelipata hamu ya kujua?”
“Sawa,” Darren akalegea. “Tutaenda huko hiyo kesho.”
Basi baada ya hapo wakafanya mpango wa chakula, wakawasha pia na runinga watazame baadhi ya filamu. Wakachoma hapo masaa mpaka kiza kilipoingia. Wakala na kuendelea kutazama runinga wakiwa wanapeana mabusu na maneno matamu. 
Usiku ulipokuwa mkubwa zaidi wakaenda kitandani, na kabla ya kulala ‘wakanyooshana migongo’. Wakachoka sana na basi usingizi ukawakwapua kwa upesi sana wasidumu hata lisaa.
Wakiwa wamelala, ni saa tisa ya usiku, ghafla Melissa anaamka na kuketi kitako kitandani. Kuna jambo linamtatiza kichwani. Anamtazama Darren, yu hoi hajielewi. Basi anatoka kitandani na kwenda kuifuata ile picha ya Bibi pale mezani. 
Akaiteka kwa mikono yake membamba kisha akairejea kuitazama kwa macho yake makavu pamoja na kiza. Baada ya sekunde mbili, akasema kwa kunong’ona, “Tabitha … Cassandra … Bessie.!”
Akisema majina hayo akawa anamtazama mmoja baada ya mwingine. Punde akasikia Darren akijigeuza kitandani, upesi akatazama. Mwanaume huyo hakuwa ameamka. Bado alikuwa kwenye lindi kubwa la usingizi. Melissa akaachana naye na kuendelea kutazama ile picha, mwishowe akaiweka kifuani mwake akiwa na uso wa mawazo.
“Tabitha, nangoja jua lichomoze,” akasema hivyo na basi akarejea kitandani mwake na kulala.
Masaa yakazidi kusonga mpaka kufikia majira ya saa kumi na moja. Hapo Darren akashtuka toka usingizini na kuangaza. Alidhani pengine amekawia. Akafungua dirisha na kutazama nje, bado kiza. Basi kabla hajajirudisha kitandani akaenda chooni kwa haja ndogo.
Alipotoka huko, kama bahati tu, akajikuta macho yake yakiangukia mezani pale alipoacha picha yake. Akasonga karibu na kuitazama tena picha ile akitumia msaada wa taa ndogo ya mezani. 
Akajikuta anatabasamu kumwona mtu mithili ya Melissa. Ila alipoitazama picha hiyo zaidi akagundua yule Melissa wa pichani alikuwa ana kovu dogo chini ya goti lake la kushoto. Aliweza kuona hivyo maana gauni lilikuwa limeishia magotini. 
Basi kwa hamu ya kutaka kujua akamsogelea Melissa kitandani kisha akamtazama mguu wake wa kushoto. Hapo akaona kovu lile lile la kwenye picha! Ni kovu dogo ambalo hakupata hata kulijua kwa muda wote huo ambao amekuwa na Melissa kwenye mahusiano.
“Inawezekanaje?” akajiuliza. Akairejesha picha ile mezani kisha akazima taa na kurejea kitandani. Akalala nyuma ya mgongo wa Melissa aliyekuwa amelala kiubavu na kidogo akapitiwa na usingizi. 
Ila hapo Melissa akafungua macho. Macho yake yalikuwa makavu tofauti na mtu atokaye usingizini. Melissa hakuwa amelala. Melissa alisikia na kuona kila kitu ambacho Darren ametoka kukifanya.
Hakufanya kitu na badala yake akalala. Asubuhi ya saa moja kamili wakaamka na kujiandaa kwa ajili ya safari. Kufikia saa tatu tayari wapo kwenye basi wakienda kijijini, countryside. 
Walipopoteza masaa matatu barabarani wakafika kituoni. Wakatembea kwa ufupi kabla ya kufika kwenye nyumba kubwa ya Bibi. Hapo Melissa akasimama kuitazama nyumba hiyo kwa umakini. Naye Darren aliyekuwa ametangulia mbele ikamlazimu amrejelee, akatabasamu akimwambia, “Ndiyo hapa! … ni pazuri, sio?” 
“Ndio, ni pazuri!” Melissa akajibu pasipo kumaanisha kwa uso wake, wakazama ndani. Humo akang’aza sana macho, ndani ya nyumba nzima na pia huko nje kana kwamba mtu anayetaka kununua akitaka kubaini madhaifu.
Walipokuwa nje, akamwomba Darren amwonyeshe kaburi la Bibi yake. Naye Darren pasipo ajizi, akampeleka magharibi ya mbali ya nyumba hiyo na kumwonyeshea, “Ndiyo hapa!”
Melissa akasoma kibao cha kaburi. Kilisomeka kwa jina la Cecilia Goodwin. Akauliza, “hili ndilo jina la bibi yako?”
“Ndio,” Darren akamjibu. 
“Ahsante. Tunaweza tukarudi ndani.” 
Wakarudi huko na Darren akampatia Melissa picha za Bibi yake. Kwa taratibu akazitazama moja baada ya nyingine. 
“Sikumwona mtu huyo tena,” alisema Darren. “Yupo kwenye picha moja tu.”
Melissa asiseme kitu akaendelea kukagua picha zile. Alipomaliza akamkabidhi Darren na kisha akalaza kichwa chake kochini. Darren akazirejesha picha hizo na kisha kujumuika na Melissa hapo sebuleni. 
Usiku ulipowadia, Melissa akamnong’oneza Darren kwenye sikio lake la kulia, “Nakuhitaji mpenzi.”
Darren akamtazama mwanamke huyo kwa kukodoa, “Melissa, tumefanya jana tu!”
Melissa akang’ata lips zake na kulegeza macho. “Kwani kuna ubaya, mpenzi?” akauliza akiweka kiganja chake kifuani mwa Darren.
“Hamna ubaya ila si kawaida yako.”
Melissa akatabasamu. Akafungua kifungo kimoja cha shati la Darren. “Sasa nitafanya nini na ingali u karibu yangu, tena tukiwa wapweke wenye nafasi?” akateta kwa sauti ya puani.
Darren asijibu, mwanamke huyo akaanza kubusu kifua chake na hatimaye akatimiza adhma yake. Darren akawa hoi kana kwamba amelima ekari  za mbaazi. Hata alipojilaza hapo kochini akawa kama mfu!
Basi Melissa akajivalia nguoze na kisha akaelekea stoo. Huko akateka chepe na kutoka ndani ya nyumba kisha akaelekea moja kwa moja kule mashariki ya mbali kukuta kaburi la Cecilia Goodwin, bibi yake Darren. 
Hapo kabla hajafanya chochote akaita kwa kunong’oneza, “Tabitha!”
Kisha akaanza kuchimba kaburi.



ITAENDELEA.......


TUPATIE NYOTA 5 KWENYE APP YETU KULE PLAY STORE NA KU COMMENT ILI TUPATE SUPPORT YAKO.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: BINAMU 🔞 SEHEMU YA 11

KIJIJINI KWA BIBI SEHEMU YA 1-5

CHOMBEZO: MASSAGE ROOM🔞 SEHEMU YA 21