BEYOND LOVE ZAIDI YA MAPENZI SEHEMU YA 21



SIMULIZI: BEYOND LOVE ZAIDI YA MAPENZI

SEHEMU YA 21

“Ndiyo...lazima niwe makini sana hapa, nikicheza hapa naweza kupoteza muelekeo wa maisha yangu! Napaswa kuwa mjanja huku nikiiacha akili yangu ichanganue mambo kwa nafasi, vinginevyo nitakuwa nakaribisha machozi tena katika maisha yangu, jambo ambalo napingana nalo kwa nguvu zote!” Aliwaza Tom.

“Lakini hapa sina ujanja tena, nimeamini hakuna mapenzi ya kweli, ni bora nikarudiana na Mariam wangu, ambaye ana mapenzi ya dhati na mimi, kwanza alinipenda kabla sijawa na kitu, kwanini nisiamini kama ananipenda?

“Nisidanganyike na hawa wasichana wa mjini, watanipotezea mwelekeo wa maisha yangu, nitakuja kulia halafu niishie kuchekwa na wabaya wangu. Mariam...Mariam wangu, tafadhali sikia kilio changu, ni kweli nimekukosea, lakini lazima ukumbuke hii dunia ina vishawishi vingi sana.

“Nilipoteza mawasiliano na wewe mpenzi wangu, sikujua kama ulipata matatizo makubwa kiasi ulichonieleza. Akili yangu ilinituma kwamba umeamua kunisusa na kumuacha baba yangu afe wakati wewe ukiwa katika matatizo makubwa.

“Nisamehe tafadhali, nisamehe mpenzi wangu na ninakuomba unikaribishe katika himaya ya mapenzi yako tena. Nisamehe mpenzi wangu, kukosea ni ukamilifu wa binadamu...tafadhali....nipo chini ya miguu yako....” akiwa anawaza hayo, ghafla mlango wa wodi aliyokuwa amelazwa ukafunguliwa.

Macho yake yakakutana na ya Juliana akimwangalia kwa huzuni huku machozi yakianza kumlengalenga! Mikononi mwake alikuwa amebeba maua mazuri yenye rangi nyeupe. Akasogea hadi kitandani alipokuwa amelala Tom, akapiga magoti chini huku mikono yake iliyobeba maua akiwa ameielekeza kwa Tom. Muda wote huo Tom alikuwa kimya akimtizama, hakunyanyua mdomo wake wala kufanya jambo lolote zaidi ya kumwangalia.

“Najua nimekukosea sana mpenzi wangu, kumbuka kwamba mimi ni binadamu, naomba unisamehe!” Juliana akasema akilia kwa uchungu.

“Nikusamehe?” Tom akauliza kwa sauti ya upole sana.

“Ndiyo naomba unisamehe mpenzi wangu, kwanza kumbuka kwamba Joseph alinilazimisha, nilipoona anazidi kuning’ang’ania nikamwacha!”

“Kwahiyo kila mtu akija kukulazimisha wakati mimi sipo utakuwa tayari kufanya naye uchafu kama mliofanya na Joseph siyo?”

“Sina maana hiyo mpenzi wangu!”

“Kumbe una maana gani?”

“Nilipitiwa mpenzi wangu, naomba unisamehe tafadhali!”

“Naomba kukuuliza swali moja la msingi sana!”

“Nakusikia!”

“Unafahamu kwamba wiki ijayo tutatakiwa kupanda madhabahuni kufunga ndoa?”

“Najua!”

“Sasa kuna ndoa gani ambayo kabla hata haijafungwa imeshaanza kuwa na usaliti?”

“Mpenzi wangu kumbuka tutaingia aibu sana kama tusipofunga, tumealika watu wengi sana na isitoshe wanatuheshimu sana, sasa tutaficha wapi nyuso zetu mpenzi wangu?”

“Jiulize wewe utauficha wapi uso wako siyo mimi!”

“Najua sweetie ndiyo maana nakuomba msamaha! Kumbuka wazazi wangu wananipenda na kuniamini sana, wakisikia nimefanya mambo haya itakuwa aibu kubwa sana kwangu na kwa familia nzima kwa ujumla, naomba unisamehe tafadhali!”

“Sawa, nimeshakusamehe!” Tom akasema huku akilia, maumivu aliyokuwa nayo moyoni mwake yalikuwa makali sana.

“Kweli Tom? Umenisamehe kweli mpenzi wangu?”

“Niamini mpenzi, ni kweli nimekusamehe!”

“Nashukuru sana kusikia hivyo!”

“Hata mimi pia, lakini lazima uwe makini na jambo moja!”

“Nakusikia mpenzi wangu!”

“Siku nikukufumania kwa mara nyingine, ujue itakuwa ndiyo mwisho wa penzi letu!”

“Nimekuelewa!”

“Siyo uelewe pekee, uweke akilini mwako na uhakikishe hurudii kosa hilo tena!”

“Nakuahidi mpenzi wangu!” Juliana akaondoka hospitalini pale akiwa na furaha sana.

Taratibu za sherehe zikaendelea kama kawaida, Juliana alikuwa na hamu sana ya kufunga ndoa na Tom, alikuwa kijana mwenye mafanikio makubwa sana. Ndoa yao ilipangwa kufungwa kifahari sana, kwanza ingefungiwa katikati ya bahari wakiwa kwenye meli na sherehe nzima ya ndoa yao ingemalizikia huko. Furaha yake ikarejea kwa mara ya pili.

“Nashukuru sana Mungu amenisaidia, Tom wangu amenisamehe, nilikuwa na mashaka sana juu ya mpenzi wangu, sikuwa na uhakika wa kurudi tena katika himaya yake, hasa ndoa ambayo ilitaka kuingia dosari.

“Lakini na mimi nimezidi tamaa, Joseph ana nini kiasi cha kunichanganya akili yangu kiasi kile? Hata hivyo, sina sababu ya kuwaza mambo yaliyopita, acha niyaache yaliyopita yaende zake na mimi nibaki na maisha yangu nikisubiria ndoa yangu iliyopo mbele yangu!” Juliana akawaza huku akitabsamu.

*****

Siku iliyofuata Tom aliruhusiwa kurudi nyumbani baada ya afya yake kutengemaa, Juliana ndiye aliyeenda kumchukua hospitalini na kumrudisha nyumbani, njiani wakizungumza mambo mengi yaliyohusu ndoa yao.

Kila mmoja alionekana kuwa na hamu sana na ndoa yao, wakawa wanakwenda Kanisani kwa ajili ya Mafundisho ya Ndoa kama kawaida, wageni wengi walikuwa wamealikwa kwa ajili ya kwenda kushuhudia ndoa hiyo ya aina yake iliyopangwa kufanyika kwenye meli.

Kila kitu kilikwenda sawa ingawa Tom alikuwa na maumivu makali sana katika moyo wake, alikuwa akiwaza sana juu ya mabaya aliyofanyiwa na Juliana. Siku aliyomkuta Joseph ambaye alikuwa rafiki yake kipenzi kifuani mwa Juliana, ilijirudia akilini mwake kila wakati huku akihisi maumivu makali sana ya mapenzi.

Walishirikiana kwa kila kitu, lakini Tom alikataa kufanya mapenzi na Juliana kwa kisingizio kwamba anasubiri hadi siku ya ndoa.

“Lakini mbona tumekuwa tukifanya siku zote hizo?”

“Siyo sababu!”

“Ni sababu!”

“Siyo sababu mpenzi wangu, unajua hata kama tumemkosea Mungu kwa siku zote hizo, halafu tumekuja kugundua baadaye kwamba tulikuwa tunamkosea ni vizuri tukabadilika!”

“Hapana...!”

“Nataka niwe na wewe mpenzi wangu, kumbuka siku ya ndoa huwa na mshawasha wake, isitoshe tutakwenda fungate, huoni kwamba itakuwa siku nzuri kwa sisi kufanya mapenzi tena, halafu isitoshe wakati huo tutaita tendo la ndoa nadhani itakuwa nzuri sana!”

“Sawa lakini moyo wangu bado una maswali mengi sana!”

“Maswali ya nini?”

“Nahisi kama kuna kitu kinaendelea moyoni mwako!”

“Acha wasiwasi wako mpenzi wangu, nini hicho kinaendelea moyoni mwangu?”

“Basi tuachane na hayo!”

“Sawa basi, tulale!”

“Mwaaa!” Wakapeana mabusu motomoto na kulala.

*******

Zikiwa zimebaki siku tatu tu kabla ya ndoa ya Tom na Juliana, huku vyombo mbalimbali vya habari vikitangaza na kuandika juu ya ndoa hiyo ya aina yake nchini Tanzania, Tom alikuwa mwenye mawazo mengi sana. Ni kweli alikuwa akimpenda sana mpenzi wake Juliana, lakini kitendo cha usaliti kiliendelea kusafiri akilini mwake siku zote tangu siku ya tukio lile na baadaye kulazwa.

Alihisi moyo wake ulikuwa unakosa kitu muhimu sana, alimhitaji sana Mariam wake hata kama asingemuoa. Alichokifanya ni kuandaa kadi kwa ajili ya Mariam kisha akampigia simu na kumtaka aonane naye.

“Umesema unaitwa nani?”

“Thomas!”

“Tom?”

“Ndiyo!”

“Unataka kuonana na mimi?”

“Ndiyo!”

“Kuna nini?”

“Ni vizuri tuonane, siwezi kuzungumza kwenye simu!”

“Namba yangu ni nani amekupa?”

“Hilo siyo la muhimu kujua kama ambalo linanifanya nikuite!”

“Tukutane wapi sasa?”

“Nitakuja Mlimani City!”

“Wapi sasa?”

“Samaki Samaki!”

“Sawa, saa ngapi?”

“Saa mbili kamili usiku nitakuwa hapo!”

“Huwezi kufanya mapema zaidi?”

“Muda huo ni mzuri zaidi kutokana na aina ya maongezi niliyonayo!”

“Ok!”

“Kazi njema!”


ITAENDELEA..........



TUPATIE NYOTA 5 KWENYE APP YETU KULE PLAY STORE NA KU COMMENT ILI TUPATE SUPPORT YAKO.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

CHOMBEZO: BINAMU 🔞 SEHEMU YA 11

KIJIJINI KWA BIBI SEHEMU YA 1-5

CHOMBEZO: MASSAGE ROOM🔞 SEHEMU YA 21