Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2020

MUNGU ATANILIPIA:

Picha
MUNGU ATANILIPIA: Nakumbuka nililazimishwa kuolewa ila nilikubali ili kutii amri ya wazazi. Nikabahatika kupata mtoto wa kike niliyempenda sana, kwani sikuwa na raha ya kuishi na mume wangu aliyekuwa mzee sana kwa bahati mbaya mume wangu alikufa kwa ugonjwa wa kisukari. Nikabaki mimi na binti yangu kwakweli sikutaka kuolewa tena niliamua kukaa na kulea mwanangu huyu. Kweli nilimlea na kumsomesha binti yangu, alipofika chuo ndipo mambo yalipoanza kubadilika. Binti yangu akanitaarifu kuwa amepata mchumba na akaja nae nyumbani kumtambulisha kwa ushamba wangu nikashangaa kweli ile gari ya mchumba wa mwanangu na nikaona raha kwa binti yangu kumpata mwanaume mwenye pesa kama yule, ilikuwa ni kipindi cha likizo na yule bwana alikuwa akija mara kwa mara kutusalimia huku akibeba zawadi tofauti tofauti, sikuwa na shaka naye hata akiniambia anataka kutoka na mwanangu nilimpa ruhusu wanaenda halafu anamrudisha nyumbani. Siku moja ambayo siwezi kuisahau kamwe katika maisha yangu, mwanangu akaniaga ...

USIWE MVIVU ISOME UTAJIFUNZA KITU

Picha
          Mtunzi: EMMANUEL MRISHO         Mwandishi: EMMANUEL MRISHO                     SIMULIZI YA KUSISIMUA  Baba mmoja alikuwa na *wake wanne.* *Alimpenda sana mke wake wa nne na alitumia gharama kubwa kwaajii yake na kumpa matunzo bora.* *Pia alimpenda mke wake wa tatu na siku zote alipenda kuwaonyesha marafiki zake mke huyu wa tatu kwakuwa alikuwa mrembo kwelikweli. Hata hivyo alikuwa na hofu kwamba huenda mke huyu anaweza msaliti aende kwa mtu mwingine kati ya hao rafiki zake.* *Pia alimpenda mke wake wa pili kwakuwa kila alipokabiliwa na matatizo mke huyu alikuwa faraja na msaada mkubwa katika kumshauri.* *Hata hivyo, huyu baba hakuwa na upendo kabisa na mke wake wa kwanza japo mke huyu alimpenda sana mume wake na alikuwa mwaminifu sana kwake.* *Siku moja yule baba aliumwa sana na alijua kwamba hana muda mrefu wa kuishi.* Akajiambia mwenyewe , *"Kwakuwa nina wake wanne nitachagua ...

USIMDHARAU USIYOYAJUA

Picha
 "Usimdharau usiyemjua undani wake" Simulizi fupi ya kusisimua..   Msichana mmoja alikuwa amempenda kijana mmoja mtanashati na mcha Mungu.. Malengo yao ilikua waje kuoana baada ya muda.  Kijana huyu alijitoa sana kwa binti huyu hadi wenzie wakamuona mjinga, lakini ukweli ni kuwa alimpenda msichana yule kwa dhati. Alimtafutia kazi alipomaliza chuo, alimshauri kuhusu mipango ya maisha na alikua akimuombea kila alipopata nafasiya kuomba.  Siku moja binti alikua anasherehekea siku yake ya kuzaliwa...hivyo akaalika marafiki zake, na watu wengine muhimu akiwemo mpenzi wake.  Wageni wote walifika kwa wakati isipokua yule kijana alichelewa kidogo... Hivyo msichana akatumia muda ule ambao mpenzi wake hajafika kuwaeleza wageni namna yule kijana alivyokua wa muhimu kwake..  Akamsifia sana, akasema atamvalisha pete ya uchumba soon, na akasema siku hiyo ya birthday yake anategemea zawadi kubwa sana kutoka kwa huyo mpenzi wa nafsi yake.   Baadae kijana aka...